< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
قصیده آساف ای قوم من شریعت مرا بشنوید! گوشهای خود را به سخنان دهانم فراگیرید!۱
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
دهان خود را به مثل باز خواهم کرد به چیزهایی که از بنای عالم مخفی بود تنطق خواهم نمود.۲
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
که آنها را شنیده و دانسته‌ایم و پدران مابرای ما بیان کرده‌اند.۳
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
از فرزندان ایشان آنها راپنهان نخواهیم کرد. تسبیحات خداوند را برای نسل آینده بیان می‌کنیم و قوت او و اعمال عجیبی را که او کرده است.۴
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
زیرا که شهادتی دریعقوب برپا داشت و شریعتی در اسرائیل قرار دادو پدران ما را امر فرمود که آنها را به فرزندان خودتعلیم دهند؛۵
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
تا نسل آینده آنها را بدانند وفرزندانی که می‌بایست مولود شوند تا ایشان برخیزند و آنها را به فرزندان خود بیان نمایند؛۶
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
و ایشان به خدا توکل نمایند و اعمال خدا رافراموش نکنند بلکه احکام او را نگاه دارند.۷
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
ومثل پدران خود نسلی گردن کش و فتنه انگیزنشوند، نسلی که دل خود را راست نساختند وروح ایشان بسوی خدا امین نبود.۸
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
بنی افرایم که مسلح و کمان کش بودند، درروز جنگ رو برتافتند.۹
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
عهد خدا را نگاه نداشتند و از سلوک به شریعت او ابا نمودند،۱۰
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
واعمال و عجایب او را فراموش کردند که آنها رابدیشان ظاهر کرده بود،۱۱
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
و در نظر پدران ایشان اعمال عجیب کرده بود، در زمین مصر و در دیارصوعن.۱۲
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
دریا را منشق ساخته، ایشان را عبورداد و آبها را مثل توده برپا نمود.۱۳
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
و ایشان را درروز به ابر راهنمایی کرد و تمامی شب به نورآتش.۱۴
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
در صحرا صخره‌ها را بشکافت و ایشان را گویا از لجه های عظیم نوشانید.۱۵
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
پس سیلها رااز صخره بیرون آورد و آب را مثل نهرها جاری ساخت.۱۶
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
و بار دیگر بر او گناه ورزیدند و برحضرت اعلی در صحرا فتنه انگیختند،۱۷
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
و دردلهای خود خدا را امتحان کردند، چونکه برای شهوات خود غذا خواستند.۱۸
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
و بر‌ضد خداتکلم کرده، گفتند: «آیا خدا می‌تواند در صحراسفره‌ای حاضر کند؟۱۹
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
اینک صخره را زد و آبهاروان شد و وادیها جاری گشت. آیا می‌تواند نان رانیز بدهد. و گوشت را برای قوم خود حاضرسازد؟»۲۰
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
پس خدا این را شنیده، غضبناک شد و آتش در یعقوب افروخته گشت و خشم بر اسرائیل مشتعل گردید.۲۱
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
زیرا به خدا ایمان نیاوردند و به نجات او اعتماد ننمودند.۲۲
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
پس ابرها را از بالاامر فرمود و درهای آسمان را گشود۲۳
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
و من را برایشان بارانید تا بخورند و غله آسمان را بدیشان بخشید.۲۴
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
مردمان، نان زورآوران را خوردند وآذوقه‌ای برای ایشان فرستاد تا سیر شوند.۲۵
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
بادشرقی را در آسمان وزانید و به قوت خود، بادجنوبی را آورد،۲۶
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
و گوشت را برای ایشان مثل غبار بارانید و مرغان بالدار را مثل ریگ دریا.۲۷
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
وآن را در میان اردوی ایشان فرود آورد، گرداگردمسکن های ایشان.۲۸
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
پس خوردند و نیکو سیرشدند و موافق شهوات ایشان بدیشان داد.۲۹
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
ایشان از شهوت خود دست نکشیدند. و غذاهنوز در دهان ایشان بود۳۰
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
که غضب خدا برایشان افروخته شده؛ تنومندان ایشان را بکشت وجوانان اسرائیل را هلاک ساخت.۳۱
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
با وجود این همه، باز گناه ورزیدند و به اعمال عجیب او ایمان نیاوردند.۳۲
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
بنابراین، روزهای ایشان را در بطالت تمام کرد و سالهای ایشان را درترس.۳۳
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
هنگامی که ایشان را کشت اورا طلبیدند و بازگشت کرده، درباره خدا تفحص نمودند،۳۴
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
و به یاد آوردند که خدا صخره ایشان، و خدای تعالی ولی ایشان است.۳۵
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
اما به دهان خود او را تملق نمودند و به زبان خویش به اودروغ گفتند.۳۶
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
زیرا که دل ایشان با او راست نبودو به عهد وی موتمن نبودند.۳۷
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
اما او به حسب رحمانیتش گناه ایشان راعفو نموده، ایشان را هلاک نساخت بلکه بارهاغضب خود را برگردانیده، تمامی خشم خویش را برنینگیخت.۳۸
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
و به یاد آورد که ایشان بشرند، بادی که می‌رود و بر نمی گردد.۳۹
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
چند مرتبه درصحرا بدو فتنه انگیختند و او را در بادیه رنجانیدند.۴۰
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
و برگشته، خدا را امتحان کردند وقدوس اسرائیل را اهانت نمودند،۴۱
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
و قوت او رابه‌خاطر نداشتند، روزی که ایشان را از دشمن رهانیده بود.۴۲
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
که چگونه آیات خود را در مصرظاهر ساخت و معجزات خود را در دیار صوعن.۴۳
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
و نهرهای ایشان را به خون مبدل نمود ورودهای ایشان را تا نتوانستند نوشید.۴۴
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
انواع پشه‌ها در میان ایشان فرستاد که ایشان را گزیدند وغوکهایی که ایشان را تباه نمودند؛۴۵
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
و محصول ایشان را به کرم صد پا سپرد و عمل ایشان را به ملخ داد.۴۶
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
تاکستان ایشان را به تگرگ خراب کردو درختان جمیز ایشان را به تگرگهای درشت.۴۷
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
بهایم ایشان را به تگرگ سپرد و مواشی ایشان را به شعله های برق.۴۸
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
و آتش خشم خود را برایشان فرستاد، غضب و غیظ و ضیق را، به فرستادن فرشتگان شریر.۴۹
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
و راهی برای غضب خود مهیا ساخته، جان ایشان را از موت نگاه نداشت، بلکه جان ایشان را به وبا تسلیم نمود.۵۰
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
و همه نخست زادگان مصر را کشت، اوایل قوت ایشان را در خیمه های حام.۵۱
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
و قوم خود را مثل گوسفندان کوچانید وایشان را در صحرا مثل گله راهنمایی نمود.۵۲
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
وایشان را در امنیت رهبری کرد تا نترسند و دریادشمنان ایشان را پوشانید.۵۳
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
و ایشان را به حدودمقدس خود آورد، بدین کوهی که به‌دست راست خود تحصیل کرده بود.۵۴
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
و امت‌ها را از حضورایشان راند و میراث را برای ایشان به ریسمان تقسیم کرد و اسباط اسرائیل را در خیمه های ایشان ساکن گردانید.۵۵
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
لیکن خدای تعالی را امتحان کرده، بدو فتنه انگیختند و شهادات او را نگاه نداشتند.۵۶
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
وبرگشته، مثل پدران خود خیانت ورزیدند و مثل کمان خطا کننده منحرف شدند.۵۷
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
و به مقامهای بلند خود خشم او را به هیجان آوردند و به بتهای خویش غیرت او را جنبش دادند.۵۸
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
چون خدااین را بشنید غضبناک گردید و اسرائیل را به شدت مکروه داشت.۵۹
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
پس مسکن شیلو را ترک نمود، آن خیمه‌ای را که در میان آدمیان برپاساخته بود،۶۰
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
و (تابوت ) قوت خود را به اسیری داد و جمال خویش را به‌دست دشمن سپرد،۶۱
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
وقوم خود را به شمشیر تسلیم نمود و با میراث خود غضبناک گردید.۶۲
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
جوانان ایشان را آتش سوزانید و برای دوشیزگان ایشان سرود نکاح نشد.۶۳
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
کاهنان ایشان به دم شمشیر افتادند وبیوه های ایشان نوحه گری ننمودند.۶۴
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
آنگاه خداوند مثل کسی‌که خوابیده بودبیدار شد، مثل جباری که از شراب می‌خروشد،۶۵
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
و دشمنان خود را به عقب زد و ایشان را عارابدی گردانید.۶۶
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
و خیمه یوسف را رد نموده، سبط افرایم را برنگزید.۶۷
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
لیکن سبط یهودا رابرگزید و این کوه صهیون را که دوست می‌داشت.۶۸
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
و قدس خود را مثل کوههای بلند بنا کرد، مثل جهان که آن را تا ابدالاباد بنیاد نهاد.۶۹
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
و بنده خود داود را برگزید و او را از آغلهای گوسفندان گرفت.۷۰
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
از عقب میشهای شیرده او را آورد تاقوم او یعقوب و میراث او اسرائیل را رعایت کند.۷۱
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
پس ایشان را به حسب کمال دل خود رعایت نمود و ایشان را به مهارت دستهای خویش هدایت کرد.۷۲

< Zaburi 78 >