< Zaburi 78 >
1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
intellectus Asaph adtendite populus meus legem meam inclinate aurem vestram in verba oris mei
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
aperiam in parabola os meum eloquar propositiones ab initio
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
quanta audivimus et cognovimus ea et patres nostri narraverunt nobis
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
non sunt occultata a filiis eorum in generationem alteram narrantes laudes Domini et virtutes eius et mirabilia eius quae fecit
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
et suscitavit testimonium in Iacob et legem posuit in Israhel quanta mandavit patribus nostris nota facere ea filiis suis
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
ut cognoscat generatio altera filii qui nascentur et exsurgent et narrabunt filiis suis
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
ut ponant in Deo spem suam et non obliviscantur opera Dei et mandata eius exquirant
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
ne fiant sicut patres eorum generatio prava et exasperans generatio quae non direxit cor suum et non est creditus cum Deo spiritus eius
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
filii Effrem intendentes et mittentes arcus conversi sunt in die belli
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
non custodierunt testamentum Dei et in lege eius noluerunt ambulare
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
et obliti sunt benefactorum eius et mirabilium eius quae ostendit eis
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
coram patribus eorum quae fecit mirabilia in terra Aegypti in campo Taneos
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
interrupit mare et perduxit eos statuit aquas quasi utrem
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
et deduxit eos in nube diei et tota nocte in inluminatione ignis
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
interrupit petram in heremo et adaquavit eos velut in abysso multa
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
et eduxit aquam de petra et deduxit tamquam flumina aquas
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
et adposuerunt adhuc peccare ei in ira excitaverunt Excelsum in inaquoso
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
et temptaverunt Deum in cordibus suis ut peterent escas animabus suis
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
et male locuti sunt de Deo dixerunt numquid poterit Deus parare mensam in deserto
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
quoniam percussit petram et fluxerunt aquae et torrentes inundaverunt numquid et panem potest dare aut parare mensam populo suo
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
ideo audivit Dominus et distulit et ignis accensus est in Iacob et ira ascendit in Israhel
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
quia non crediderunt in Deo nec speraverunt in salutare eius
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
et mandavit nubibus desuper et ianuas caeli aperuit
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
et pluit illis manna ad manducandum et panem caeli dedit eis
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
panem angelorum manducavit homo cibaria misit eis in abundantiam
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
transtulit austrum de caelo et induxit in virtute sua africum
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
et pluit super eos sicut pulverem carnes et sicut harenam maris volatilia pinnata
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
et ceciderunt in medio castrorum eorum circa tabernacula eorum
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
et manducaverunt et saturati sunt nimis et desiderium eorum adtulit eis
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
non sunt fraudati a desiderio suo adhuc escae eorum erant in ore ipsorum
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
et ira Dei ascendit in eos et occidit pingues eorum et electos Israhel inpedivit
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
in omnibus his peccaverunt adhuc et non crediderunt mirabilibus eius
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
et defecerunt in vanitate dies eorum et anni eorum cum festinatione
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
cum occideret eos quaerebant eum et revertebantur et diluculo veniebant ad Deum
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
et rememorati sunt quia Deus adiutor est eorum et Deus excelsus redemptor eorum est
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
et dilexerunt eum in ore suo et lingua sua mentiti sunt ei
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
cor autem ipsorum non erat rectum cum eo nec fideles habiti sunt in testamento eius
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
ipse autem est misericors et propitius fiet peccatis eorum et non perdet eos et abundabit ut avertat iram suam et non accendet omnem iram suam
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
et recordatus est quia caro sunt spiritus vadens et non rediens
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
quotiens exacerbaverunt eum in deserto in ira concitaverunt eum in inaquoso
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
et conversi sunt et temptaverunt Deum et Sanctum Israhel exacerbaverunt
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
non sunt recordati manus eius die qua redemit eos de manu tribulantis
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
sicut posuit in Aegypto signa sua et prodigia sua in campo Taneos
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
et convertit in sanguine flumina eorum et imbres eorum ne biberent
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
misit in eos cynomiam et comedit eos et ranam et disperdit eos
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
et dedit erugini fructus eorum et labores eorum lucustae
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
et occidit in grandine vineam eorum et moros eorum in pruina
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
et tradidit grandini iumenta eorum et possessionem eorum igni
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
misit in eos iram indignationis suae indignationem et iram et tribulationem inmissionem per angelos malos
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
viam fecit semitae irae suae non pepercit a morte animarum eorum et iumenta eorum in morte conclusit
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
et percussit omne primitivum in terra Aegypti primitias laborum eorum in tabernaculis Cham
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
et abstulit sicut oves populum suum et perduxit eos tamquam gregem in deserto
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
et deduxit eos in spe et non timuerunt et inimicos eorum operuit mare
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
et induxit eos in montem sanctificationis suae montem quem adquisivit dextera eius et eiecit a facie eorum gentes et sorte divisit eis terram in funiculo distributionis
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
et habitare fecit in tabernaculis eorum tribus Israhel
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
et temptaverunt et exacerbaverunt Deum excelsum et testimonia eius non custodierunt
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
et averterunt se et non servaverunt pactum quemadmodum patres eorum conversi sunt in arcum pravum
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
et in ira concitaverunt eum in collibus suis et in sculptilibus suis ad aemulationem eum provocaverunt
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
audivit Deus et sprevit et ad nihilum redegit valde Israhel
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
et reppulit tabernaculum Selo tabernaculum suum ubi habitavit in hominibus
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
et tradidit in captivitatem virtutem eorum et pulchritudinem eorum in manus inimici
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
et conclusit in gladio populum suum et hereditatem suam sprevit
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
iuvenes eorum comedit ignis et virgines eorum non sunt lamentatae
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
sacerdotes eorum in gladio ceciderunt et viduae eorum non plorabuntur
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
et excitatus est tamquam dormiens Dominus tamquam potens crapulatus a vino
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
et percussit inimicos suos in posteriora obprobrium sempiternum dedit illis
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
et reppulit tabernaculum Ioseph et tribum Effrem non elegit
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
et elegit tribum Iuda montem Sion quem dilexit
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
et aedificavit sicut unicornium sanctificium suum in terra quam fundavit in saecula
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
et elegit David servum suum et sustulit eum de gregibus ovium de post fetantes accepit eum
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
pascere Iacob servum suum et Israhel hereditatem suam
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
et pavit eos in innocentia cordis sui et in intellectibus manuum suarum deduxit eos