< Zaburi 78 >
1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
アサフのマスキールの歌 わが民よ、わが教を聞き、わが口の言葉に耳を傾けよ。
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
わたしは口を開いて、たとえを語り、いにしえからの、なぞを語ろう。
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
これはわれらがさきに聞いて知ったこと、またわれらの先祖たちがわれらに語り伝えたことである。
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
われらはこれを子孫に隠さず、主の光栄あるみわざと、その力と、主のなされたくすしきみわざとをきたるべき代に告げるであろう。
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
主はあかしをヤコブのうちにたて、おきてをイスラエルのうちに定めて、その子孫に教うべきことをわれらの先祖たちに命じられた。
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
これは次の代に生れる子孫がこれを知り、みずから起って、そのまた子孫にこれを伝え、
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
彼らをして神に望みをおき、神のみわざを忘れず、その戒めを守らせるためである。
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
またその先祖たちのようにかたくなで、そむく者のやからとなり、その心が定まりなく、その魂が神に忠実でないやからとならないためである。
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
エフライムの人々は武装し、弓を携えたが、戦いの日に引き返した。
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
彼らは神の契約を守らず、そのおきてにしたがって歩むことを拒み、
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
神がなされた事と、彼らに示されたくすしきみわざとを忘れた。
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
神はエジプトの地と、ゾアンの野でくすしきみわざを彼らの先祖たちの前に行われた。
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
神は海を分けて彼らを通らせ、水を立たせて山のようにされた。
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
昼は雲をもって彼らを導き、夜は、よもすがら火の光をもって彼らを導かれた。
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
神は荒野で岩を裂き、淵から飲むように豊かに彼らに飲ませ、
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
また岩から流れを引いて、川のように水を流れさせられた。
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
ところが彼らはなお神にむかって罪をかさね、荒野でいと高き者にそむき、
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
おのが欲のために食物を求めて、その心のうちに神を試みた。
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
また彼らは神に逆らって言った、「神は荒野に宴を設けることができるだろうか。
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
見よ、神が岩を打たれると、水はほとばしりいで、流れがあふれた。神はまたパンを与えることができるだろうか。民のために肉を備えることができるだろうか」と。
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
それゆえ、主は聞いて憤られた。火はヤコブにむかって燃えあがり、怒りはイスラエルにむかって立ちのぼった。
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
これは彼らが神を信ぜず、その救の力を信用しなかったからである。
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
しかし神は上なる大空に命じて天の戸を開き、
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
彼らの上にマナを降らせて食べさせ、天の穀物を彼らに与えられた。
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
人は天使のパンを食べた。神は彼らに食物をおくって飽き足らせられた。
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
神は天に東風を吹かせ、み力をもって南風を導かれた。
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
神は彼らの上に肉をちりのように降らせ、翼ある鳥を海の砂のように降らせて、
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
その宿営のなか、そのすまいのまわりに落された。
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
こうして彼らは食べて、飽き足ることができた。神が彼らにその望んだものを与えられたからである。
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
ところが彼らがまだその欲を離れず、食物がなお口の中にあるうちに、
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
神の怒りが彼らにむかって立ちのぼり、彼らのうちの最も強い者を殺し、イスラエルのうちのえり抜きの者を打ち倒された。
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
すべてこれらの事があったにもかかわらず、彼らはなお罪を犯し、そのくすしきみわざを信じなかった。
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
それゆえ神は彼らの日を息のように消えさせ、彼らの年を恐れをもって過ごさせられた。
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
神が彼らを殺されたとき、彼らは神をたずね、悔いて神を熱心に求めた。
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
こうして彼らは、神は彼らの岩、いと高き神は彼らのあがないぬしであることを思い出した。
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
しかし彼らはその口をもって神にへつらい、その舌をもって神に偽りを言った。
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
彼らの心は神にむかって堅実でなく、神の契約に真実でなかった。
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
しかし神はあわれみに富まれるので、彼らの不義をゆるして滅ぼさず、しばしばその怒りをおさえて、その憤りをことごとくふり起されなかった。
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
また神は、彼らがただ肉であって、過ぎ去れば再び帰りこぬ風であることを思い出された。
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
幾たび彼らは野で神にそむき、荒野で神を悲しませたことであろうか。
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
彼らはかさねがさね神を試み、イスラエルの聖者を怒らせた。
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
彼らは神の力をも、神が彼らをあだからあがなわれた日をも思い出さなかった。
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
神はエジプトでもろもろのしるしをおこない、ゾアンの野でもろもろの奇跡をおこない、
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
彼らの川を血に変らせて、その流れを飲むことができないようにされた。
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
神ははえの群れを彼らのうちに送って彼らを食わせ、かえるを送って彼らを滅ぼされた。
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
また神は彼らの作物を青虫にわたし、彼らの勤労の実をいなごにわたされた。
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
神はひょうをもって彼らのぶどうの木を枯らし、霜をもって彼らのいちじく桑の木を枯らされた。
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
神は彼らの家畜をひょうにわたし、彼らの群れを燃えるいなずまにわたされた。
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
神は彼らの上に激しい怒りと、憤りと、恨みと、悩みと、滅ぼす天使の群れとを放たれた。
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
神はその怒りのために道を設け、彼らの魂を死から免れさせず、そのいのちを疫病にわたされた。
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
神はエジプトですべてのういごを撃ち、ハムの天幕で彼らの力の初めの子を撃たれた。
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
こうして神はおのれの民を羊のように引き出し、彼らを荒野で羊の群れのように導き、
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
彼らを安らかに導かれたので彼らは恐れることがなかった。しかし海は彼らの敵をのみつくした。
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
神は彼らをその聖地に伴い、その右の手をもって獲たこの山に伴いこられた。
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
神は彼らの前からもろもろの国民を追い出し、その地を分けて嗣業とし、イスラエルの諸族を彼らの天幕に住まわせられた。
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
しかし彼らはいと高き神を試み、これにそむいて、そのもろもろのあかしを守らず、
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
そむき去って、先祖たちのように真実を失い、狂った弓のようにねじれた。
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
彼らは高き所を設けて神を怒らせ、刻んだ像をもって神のねたみを起した。
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
神は聞いて大いに怒り、イスラエルを全くしりぞけられた。
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
神は人々のなかに設けた幕屋なるシロのすまいを捨て、
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
その力をとりことならせ、その栄光をあだの手にわたされた。
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
神はその民をつるぎにわたし、その嗣業にむかって大いなる怒りをもらされた。
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
火は彼らの若者たちを焼きつくし、彼らのおとめたちは婚姻の歌を失い、
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
彼らの祭司たちはつるぎによって倒れ、彼らのやもめたちは嘆き悲しむことさえしなかった。
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
そのとき主は眠った者のさめたように、勇士が酒によって叫ぶように目をさまして、
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
そのあだを撃ち退け、とこしえの恥を彼らに負わせられた。
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
神はヨセフの天幕をしりぞけ、エフライムの部族を選ばず、
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
ユダの部族を選び、神の愛するシオンの山を選ばれた。
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
神はその聖所を高い天のように建て、とこしえに基を定められた地のように建てられた。
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
神はそのしもべダビデを選んで、羊のおりから取り、
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
乳を与える雌羊の番をするところからつれて来て、その民ヤコブ、その嗣業イスラエルの牧者とされた。
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
こうして彼は直き心をもって彼らを牧し、巧みな手をもって彼らを導いた。