< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Ein Lehrgedicht von Asaph. Gib acht, mein Volk, auf meine Belehrung,
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Ich will auftun meinen Mund zur Rede in Sprüchen, will Rätsel verkünden von der Vorzeit her.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Was wir gehört und erfahren und unsere Väter uns erzählt haben,
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
das wollen wir ihren Kindern nicht verschweigen, sondern dem künftgen Geschlecht verkünden die Ruhmestaten des HERRN und seine Stärke und die Wunder, die er getan hat.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Denn er hat ein Zeugnis aufgerichtet in Jakob und festgestellt in Israel ein Gesetz, von dem er unsern Vätern gebot, es ihren Kindern kundzutun,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
auf daß die Nachwelt Kenntnis davon erhielte: die Kinder, die geboren würden, sollten aufstehn und ihren Kindern davon erzählen,
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
daß sie auf Gott ihr Vertrauen setzten und die Taten Gottes nicht vergäßen und seine Gebote befolgten,
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
daß sie nicht wie ihre Väter würden, ein trotziges und widerspenstiges Geschlecht, ein Geschlecht mit wankelmütigem Herzen, dessen Geist sich nicht zuverlässig zu Gott hielt.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Ephraims Söhne, bogengerüstete Schützen, haben den Rücken gewandt am Tage des Kampfes.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Sie hielten den gottgestifteten Bund nicht und wollten nicht wandeln in seinem Gesetz;
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
nein, sie vergaßen seine Taten und seine Wunder, die er sie hatte sehen lassen.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Vor ihren Vätern hatte er Wunder getan im Lande Ägypten, im Gefilde von Zoan.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Er spaltete das Meer und ließ sie hindurchziehn und türmte die Wasser auf wie einen Wall;
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
er leitete sie bei Tag durch die Wolke und während der ganzen Nacht durch Feuerschein;
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
er spaltete Felsen in der Wüste und tränkte sie reichlich wie mit Fluten;
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Bäche ließ er aus dem Felsen hervorgehn und Wasser gleich Strömen niederfließen.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Dennoch fuhren sie fort, gegen ihn zu sündigen, und widerstrebten dem Höchsten in der Wüste;
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
ja, sie versuchten Gott in ihren Herzen, indem sie Speise verlangten für ihr Gelüst,
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
und redeten gegen Gott mit den Worten: »Kann Gott wohl einen Tisch in der Wüste uns decken?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Wohl hat er den Felsen geschlagen, daß Wasser flossen heraus und Bäche sich ergossen; doch wird er auch vermögen Brot zu geben oder Fleisch seinem Volke zu schaffen?«
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Drum, als der HERR das hörte, ergrimmte er: Feuer entbrannte gegen Jakob, und Zorn stieg auf gegen Israel,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
weil sie an Gott nicht glaubten und auf seine Hilfe nicht vertrauten.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Und doch gebot er den Wolken droben und tat die Türen des Himmels auf,
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
ließ Manna auf sie regnen zum Essen und gab ihnen himmlisches Brotkorn:
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Engelspeise aßen sie allesamt, Reisekost sandte er ihnen zur Sättigung.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Hinfahren ließ er den Ostwind am Himmel und führte durch seine Kraft den Südwind herbei;
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Fleisch ließ er auf sie regnen wie Staub und beschwingte Vögel wie Meeressand;
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
mitten in ihr Lager ließ er sie fallen, rings um ihre Wohnungen her.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Da aßen sie und wurden reichlich satt, und was sie gewünscht, gewährte er ihnen.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Noch hatten sie ihres Gelüsts sich nicht entschlagen, noch hatten sie ihre Speise in ihrem Munde,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
da stieg der Ingrimm Gottes gegen sie auf und erwürgte die kräftigen Männer unter ihnen und streckte Israels junge Mannschaft zu Boden.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Trotz alledem sündigten sie weiter und glaubten nicht an seine Wunder.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Drum ließ er ihre Tage vergehn wie einen Hauch und ihre Jahre in angstvoller Hast.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Wenn er sie sterben ließ, dann fragten sie nach ihm und kehrten um und suchten Gott eifrig
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
und dachten daran, daß Gott ihr Fels sei und Gott, der Höchste, ihr Erlöser.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Doch sie heuchelten ihm mit ihrem Munde und belogen ihn mit ihrer Zunge;
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
denn ihr Herz hing nicht fest an ihm, und sie hielten nicht treu an seinem Bunde.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Doch er war barmherzig, vergab die Schuld und vertilgte sie nicht, nein, immer wieder hielt er seinen Zorn zurück und ließ nicht seinen ganzen Grimm erwachen;
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
denn er dachte daran, daß Fleisch sie waren, ein Windhauch, der hinfährt und nicht wiederkehrt.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Wie oft widerstrebten sie ihm in der Wüste, kränkten sie ihn in der Öde!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Und immer aufs neue versuchten sie Gott und betrübten den Heiligen Israels.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Sie dachten nicht mehr an seine starke Hand, an den Tag, wo er sie vom Bedränger erlöste,
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
als er seine Zeichen in Ägypten tat, seine Wunder im Gefilde von Zoan.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
Er verwandelte dort in Blut ihre Ströme, so daß man ihr fließendes Wasser nicht trinken konnte;
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
er sandte unter sie Ungeziefer, das sie fraß, und Frösche, die ihnen Verderben brachten;
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
er gab ihre Ernte den Freßgrillen preis und die Frucht ihrer Arbeit den Heuschrecken;
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
er zerschlug ihre Reben mit Hagel, ihre Maulbeerfeigenbäume mit Schloßen;
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
er gab ihr Vieh dem Hagel preis und ihren Besitz den Blitzen;
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
er sandte gegen sie seines Zornes Glut, Wut und Grimm und Drangsal: eine Schar von Unglücksengeln;
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
er ließ seinem Ingrimm freien Lauf, entzog ihre Seele nicht dem Tode, überließ vielmehr ihr Leben der Pest;
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
er ließ alle Erstgeburt in Ägypten sterben, der Manneskraft Erstlinge in den Zelten Hams.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Dann ließ er sein Volk ausziehn wie Schafe und leitete sie in der Wüste wie eine Herde
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
und führte sie sicher, so daß sie nicht bangten; ihre Feinde aber bedeckte das Meer.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
So brachte er sie nach seinem heiligen Gebiet, in das Bergland, das er mit seiner Rechten erworben,
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
und vertrieb vor ihnen her die Völker, verloste ihr Gebiet als erblichen Besitz und ließ in ihren Zelten die Stämme Israels wohnen.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Doch sie versuchten und reizten Gott, den Höchsten, und hielten sich nicht an seine Gebote,
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
sondern fielen ab und handelten treulos, ihren Vätern gleich; sie versagten wie ein trüglicher Bogen
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
und erbitterten ihn durch ihren Höhendienst und reizten ihn zum Eifer durch ihre Götzenbilder.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Als Gott es vernahm, ergrimmte er und verwarf Israel ganz und gar:
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
er gab seine Wohnung in Silo auf, das Zelt, das er aufgeschlagen unter den Menschen;
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
er ließ seine Macht in Gefangenschaft fallen und seine Zier in die Hand des Feindes;
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
er gab sein Volk dem Schwerte preis und war entrüstet über sein Erbteil;
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
seine jungen Männer fraß das Feuer, und seine Jungfraun blieben ohne Brautlied;
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
seine Priester fielen durchs Schwert, und seine Witwen konnten keine Totenklage halten.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Da erwachte der Allherr wie ein Schlafender, wie ein vom Wein übermannter Kriegsheld;
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
er schlug seine Feinde von hinten und gab sie ewiger Schande preis.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Auch verwarf er das Zelt Josephs und erwählte nicht den Stamm Ephraim,
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
sondern erwählte den Stamm Juda, den Berg Zion, den er liebgewonnen;
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
und er baute den ragenden Bergen gleich sein Heiligtum, fest wie die Erde, die er auf ewig gegründet.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Dann erwählte er David, seinen Knecht, den er wegnahm von den Hürden des Kleinviehs;
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
von den Mutterschafen holte er ihn, daß er Jakob weide, sein Volk, und Israel, seinen Erbbesitz.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Der weidete sie mit redlichem Herzen und leitete sie mit kundiger Hand.

< Zaburi 78 >