< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Eine Unterweisung Asaphs. Höre, mein Volk, mein Gesetz; neigt eure Ohren zu der Rede meines Mundes!
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Ich will meinen Mund auftun zu Sprüchen und alte Geschichten aussprechen,
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
die wir gehört haben und wissen und unsre Väter uns erzählt haben,
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
daß wir's nicht verhalten sollten ihren Kindern, die hernach kommen, und verkündigten den Ruhm des HERRN und seine Macht und seine Wunder, die er getan hat.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Er richtete ein Zeugnis auf in Jakob und gab ein Gesetz in Israel, das er unsern Vätern gebot zu lehren ihre Kinder,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
auf daß es die Nachkommen lernten und die Kinder, die noch sollten geboren werden; wenn sie aufkämen, daß sie es auch ihren Kinder verkündigten,
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
daß sie setzten auf Gott ihre Hoffnung und nicht vergäßen der Taten Gottes und seine Gebote hielten
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
und nicht würden wie ihre Väter, eine abtrünnige und ungehorsame Art, welchen ihr Herz nicht fest war und ihr Geist nicht treulich hielt an Gott,
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
wie die Kinder Ephraim, die geharnischt den Bogen führten, abfielen zur Zeit des Streits.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Sie hielten den Bund Gottes nicht und wollten nicht in seinem Gesetz wandeln
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
und vergaßen seiner Taten und seiner Wunder, die er ihnen erzeigt hatte.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Vor ihren Vätern tat er Wunder in Ägyptenland, im Felde Zoan.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Er zerteilte das Meer und ließ sie hindurchgehen und stellte das Wasser wie eine Mauer.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Er leitete sie des Tages mit einer Wolke und des Nachts mit einem hellen Feuer.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Er riß die Felsen in der Wüste und tränkte sie mit Wasser die Fülle
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
und ließ Bäche aus den Felsen fließen, daß sie hinabflossen wie Wasserströme.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Dennoch sündigten sie weiter gegen ihn und erzürnten den Höchsten in der Wüste
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
und versuchten Gott in ihrem Herzen, daß sie Speise forderten für ihre Seelen,
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
und redeten gegen Gott und sprachen: “Ja, Gott sollte wohl können einen Tisch bereiten in der Wüste?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Siehe, er hat wohl den Felsen geschlagen, daß Wasser flossen und Bäche sich ergossen; aber wie kann er Brot geben und seinem Volke Fleisch verschaffen?”
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Da nun das der HERR hörte, entbrannte er, und Feuer ging an in Jakob, und Zorn kam über Israel,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
daß sie nicht glaubten an Gott und hofften nicht auf seine Hilfe.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Und er gebot den Wolken droben und tat auf die Türen des Himmels
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
und ließ das Man auf sie regnen, zu essen, und gab ihnen Himmelsbrot.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Sie aßen Engelbrot; er sandte ihnen Speise die Fülle.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Er ließ wehen den Ostwind unter dem Himmel und erregte durch seine Stärke den Südwind
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
und ließ Fleisch auf sie regnen wie Staub und Vögel wie Sand am Meer
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
und ließ sie fallen unter ihr Lager allenthalben, da sie wohnten.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Da aßen sie und wurden allzu satt; er ließ sie ihre Lust büßen.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Da sie nun ihre Lust gebüßt hatten und noch davon aßen,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
da kam der Zorn Gottes über sie und erwürgte die Vornehmsten unter ihnen und schlug darnieder die Besten in Israel.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Aber über das alles sündigten sie noch mehr und glaubten nicht an seine Wunder.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Darum ließ er sie dahinsterben, daß sie nichts erlangten und mußten ihr Leben lang geplagt sein.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Wenn er sie erwürgte, suchten sie ihn und kehrten sich zu Gott
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
und gedachten, daß Gott ihr Hort ist und Gott der Höchste ihr Erlöser ist,
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
und heuchelten mit ihrem Munde und logen ihm mit ihrer Zunge;
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
aber ihr Herz war nicht fest an ihm, und hielten nicht treulich an seinem Bund.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Er aber war barmherzig und vergab die Missetat und vertilgte sie nicht und wandte oft seinen Zorn ab und ließ nicht seinen ganzen Zorn gehen.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Denn er gedachte, daß sie Fleisch sind, ein Wind, der dahinfährt und nicht wiederkommt.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Wie oft erzürnten sie ihn in der Wüste und entrüsteten ihn in der Einöde!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Sie versuchten Gott immer wieder und meisterten den Heiligen in Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Sie gedachten nicht an seine Hand des Tages, da er sie erlöste von den Feinden;
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
wie er denn seine Zeichen in Ägypten getan hatte und seine Wunder im Lande Zoan;
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
da er ihr Wasser in Blut wandelte, daß sie ihre Bäche nicht trinken konnten;
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
da er Ungeziefer unter sie schickte, daß sie fraß, und Frösche, die sie verderbten,
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
und gab ihre Gewächse den Raupen und ihre Saat den Heuschrecken;
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
da er ihre Weinstöcke mit Hagel schlug und ihre Maulbeerbäume mit Schloßen;
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
da er ihr Vieh schlug mit Hagel und ihre Herden mit Wetterstrahlen;
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
da er böse Engel unter sie sandte in seinem grimmigen Zorn und ließ sie toben und wüten und Leid tun;
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
da er seinen Zorn ließ fortgehen und ihre Seele vor dem Tode nicht verschonte und übergab ihr Leben der Pestilenz;
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
da er alle Erstgeburt in Ägypten schlug, die Erstlinge ihrer Kraft in den Hütten Hams,
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
und ließ sein Volk ausziehen wie die Schafe und führte sie wie eine Herde in der Wüste.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Und leitete sie sicher, daß sie sich nicht fürchteten; aber ihre Feinde bedeckte das Meer.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Und er brachte sie zu seiner heiligen Grenze, zu diesem Berge, den seine Rechte erworben hat,
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
und vertrieb vor ihnen her die Völker und ließ ihnen das Erbe austeilen und ließ in jener Hütten die Stämme Israels wohnen.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Aber sie versuchten und erzürnten Gott den Höchsten und hielten ihre Zeugnisse nicht
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
und fielen zurück und verachteten alles wie ihre Väter und hielten nicht, gleichwie ein loser Bogen,
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
und erzürnten ihn mit ihren Höhen und reizten ihn mit ihren Götzen.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Und da das Gott hörte, entbrannte er und verwarf Israel ganz,
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
daß er seine Wohnung zu Silo ließ fahren, die Hütte, da er unter Menschen wohnte,
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
und gab seine Macht ins Gefängnis und seine Herrlichkeit in die Hand des Feindes
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
und übergab sein Volk ins Schwert und entbrannte über sein Erbe.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Ihre junge Mannschaft fraß das Feuer, und ihre Jungfrauen mußten ungefreit bleiben.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Ihre Priester fielen durchs Schwert, und waren keine Witwen, die da weinen sollten.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Und der Herr erwachte wie ein Schlafender, wie ein Starker jauchzt, der vom Wein kommt,
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
und schlug seine Feinde zurück und hängte ihnen ewige Schande an.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Und er verwarf die Hütte Josephs und erwählte nicht den Stamm Ephraim,
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
sondern erwählte den Stamm Juda, den Berg Zion, welchen er liebte.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Und baute sein Heiligtum hoch, wie die Erde, die ewiglich fest stehen soll.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Und erwählte seinen Knecht David und nahm ihn von den Schafställen;
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
von den säugenden Schafen holte er ihn, daß er sein Volk Jakob weiden sollte und sein Erbe Israel.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Und er weidete sie auch mit aller Treue und regierte mit allem Fleiß.

< Zaburi 78 >