< Zaburi 78 >
1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Cantique d’Asaph. Mon peuple, écoute mes instructions! Prêtez l’oreille aux paroles de ma bouche!
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
J’ouvre la bouche par des sentences, Je publie la sagesse des temps anciens.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Ce que nous avons entendu, ce que nous savons, Ce que nos pères nous ont raconté,
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
Nous ne le cacherons point à leurs enfants; Nous dirons à la génération future les louanges de l’Éternel, Et sa puissance, et les prodiges qu’il a opérés.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Il a établi un témoignage en Jacob, Il a mis une loi en Israël, Et il a ordonné à nos pères de l’enseigner à leurs enfants,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
Pour qu’elle fût connue de la génération future, Des enfants qui naîtraient, Et que, devenus grands, ils en parlassent à leurs enfants,
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
Afin qu’ils missent en Dieu leur confiance, Qu’ils n’oubliassent pas les œuvres de Dieu, Et qu’ils observassent ses commandements,
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
Afin qu’ils ne fussent pas, comme leurs pères, Une race indocile et rebelle, Une race dont le cœur n’était pas ferme, Et dont l’esprit n’était pas fidèle à Dieu.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Les fils d’Éphraïm, armés et tirant de l’arc, Tournèrent le dos le jour du combat.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Ils ne gardèrent point l’alliance de Dieu, Et ils refusèrent de marcher selon sa loi.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Ils mirent en oubli ses œuvres, Ses merveilles qu’il leur avait fait voir.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Devant leurs pères il avait fait des prodiges, Au pays d’Égypte, dans les campagnes de Tsoan.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Il fendit la mer et leur ouvrit un passage, Il fit dresser les eaux comme une muraille.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Il les conduisit le jour par la nuée, Et toute la nuit par un feu éclatant.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Il fendit des rochers dans le désert, Et il donna à boire comme des flots abondants;
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Du rocher il fit jaillir des sources, Et couler des eaux comme des fleuves.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Mais ils continuèrent à pécher contre lui, A se révolter contre le Très-Haut dans le désert.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Ils tentèrent Dieu dans leur cœur, En demandant de la nourriture selon leur désir.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Ils parlèrent contre Dieu, Ils dirent: Dieu pourrait-il Dresser une table dans le désert?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Voici, il a frappé le rocher, et des eaux ont coulé, Et des torrents se sont répandus; Pourra-t-il aussi donner du pain, Ou fournir de la viande à son peuple?
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
L’Éternel entendit, et il fut irrité; Un feu s’alluma contre Jacob, Et la colère s’éleva contre Israël,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
Parce qu’ils ne crurent pas en Dieu, Parce qu’ils n’eurent pas confiance dans son secours.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Il commanda aux nuages d’en haut, Et il ouvrit les portes des cieux;
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
Il fit pleuvoir sur eux la manne pour nourriture, Il leur donna le blé du ciel.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Ils mangèrent tous le pain des grands, Il leur envoya de la nourriture à satiété.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Il fit souffler dans les cieux le vent d’orient, Et il amena par sa puissance le vent du midi;
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Il fit pleuvoir sur eux la viande comme de la poussière, Et comme le sable des mers les oiseaux ailés;
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
Il les fit tomber au milieu de leur camp, Tout autour de leurs demeures.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Ils mangèrent et se rassasièrent abondamment: Dieu leur donna ce qu’ils avaient désiré.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Ils n’avaient pas satisfait leur désir, Ils avaient encore leur nourriture dans la bouche,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
Lorsque la colère de Dieu s’éleva contre eux; Il frappa de mort les plus vigoureux, Il abattit les jeunes hommes d’Israël.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Malgré tout cela, ils continuèrent à pécher, Et ne crurent point à ses prodiges.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Il consuma leurs jours par la vanité, Et leurs années par une fin soudaine.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Quand il les frappait de mort, ils le cherchaient, Ils revenaient et se tournaient vers Dieu;
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Ils se souvenaient que Dieu était leur rocher, Que le Dieu Très-Haut était leur libérateur.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Mais ils le trompaient de la bouche, Et ils lui mentaient de la langue;
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
Leur cœur n’était pas ferme envers lui, Et ils n’étaient pas fidèles à son alliance.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Toutefois, dans sa miséricorde, il pardonne l’iniquité et ne détruit pas; Il retient souvent sa colère et ne se livre pas à toute sa fureur.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Il se souvint qu’ils n’étaient que chair, Un souffle qui s’en va et ne revient pas.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Que de fois ils se révoltèrent contre lui dans le désert! Que de fois ils l’irritèrent dans la solitude!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Ils ne cessèrent de tenter Dieu, Et de provoquer le Saint d’Israël.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Ils ne se souvinrent pas de sa puissance, Du jour où il les délivra de l’ennemi,
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
Des miracles qu’il accomplit en Égypte, Et de ses prodiges dans les campagnes de Tsoan.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
Il changea leurs fleuves en sang, Et ils ne purent en boire les eaux.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Il envoya contre eux des mouches venimeuses qui les dévorèrent, Et des grenouilles qui les détruisirent.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
Il livra leurs récoltes aux sauterelles, Le produit de leur travail aux sauterelles.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Il fit périr leurs vignes par la grêle, Et leurs sycomores par la gelée.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
Il abandonna leur bétail à la grêle, Et leurs troupeaux au feu du ciel.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Il lança contre eux son ardente colère, La fureur, la rage et la détresse, Une troupe de messagers de malheur.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Il donna libre cours à sa colère, Il ne sauva pas leur âme de la mort, Il livra leur vie à la mortalité;
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
Il frappa tous les premiers-nés en Égypte, Les prémices de la force sous les tentes de Cham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Il fit partir son peuple comme des brebis, Il les conduisit comme un troupeau dans le désert.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Il les dirigea sûrement, pour qu’ils fussent sans crainte, Et la mer couvrit leurs ennemis.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Il les amena vers sa frontière sainte, Vers cette montagne que sa droite a acquise.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
Il chassa devant eux les nations, Leur distribua le pays en héritage, Et fit habiter dans leurs tentes les tribus d’Israël.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Mais ils tentèrent le Dieu Très-Haut et se révoltèrent contre lui, Et ils n’observèrent point ses ordonnances.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Ils s’éloignèrent et furent infidèles, comme leurs pères, Ils tournèrent, comme un arc trompeur.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Ils l’irritèrent par leurs hauts lieux, Et ils excitèrent sa jalousie par leurs idoles.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Dieu entendit, et il fut irrité; Il repoussa fortement Israël.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
Il abandonna la demeure de Silo, La tente où il habitait parmi les hommes;
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
Il livra sa gloire à la captivité, Et sa majesté entre les mains de l’ennemi.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
Il mit son peuple à la merci du glaive, Et il s’indigna contre son héritage.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Le feu dévora ses jeunes hommes, Et ses vierges ne furent pas célébrées;
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Ses sacrificateurs tombèrent par l’épée, Et ses veuves ne pleurèrent pas.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Le Seigneur s’éveilla comme celui qui a dormi, Comme un héros qu’a subjugué le vin.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
Il frappa ses adversaires en fuite, Il les couvrit d’un opprobre éternel.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Cependant il rejeta la tente de Joseph, Et il ne choisit point la tribu d’Éphraïm;
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Il préféra la tribu de Juda, La montagne de Sion qu’il aimait.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Et il bâtit son sanctuaire comme les lieux élevés, Comme la terre qu’il a fondée pour toujours.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Il choisit David, son serviteur, Et il le tira des bergeries;
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
Il le prit derrière les brebis qui allaitent, Pour lui faire paître Jacob, son peuple, Et Israël, son héritage.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Et David les dirigea avec un cœur intègre, Et les conduisit avec des mains intelligentes.