< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Maskîl d’Assaph. Ecoute, ô mon peuple, mon enseignement, prête l’oreille aux paroles de ma bouche.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
J’Ouvre les lèvres pour des sentences poétiques, j’énonce des aphorismes venant des temps anciens.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Ce que nous connaissons pour l’avoir entendu, ce que nos pères nous ont raconté,
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
nous ne le laissons pas ignorer à leurs descendants; à la génération la plus reculée nous voulons raconter les œuvres glorieuses de l’Eternel, sa puissance et les merveilles qu’il a accomplies.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Il a établi un code dans Jacob, institué une loi en Israël; et il ordonna à nos pères de les enseigner à leurs enfants,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
pour que la génération future soit mise au courant, pour que les enfants qui viendraient à naître se lèvent et à leur tour en instruisent leurs fils.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
Qu’ils mettent donc leur confiance en Dieu, se gardent d’oublier les hauts faits du Tout-Puissant, et observent ses prescriptions!
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
Et qu’ils ne soient pas, comme leurs ancêtres, une génération insoumise et rebelle, une génération au cœur inconstant et à l’esprit non sincèrement fidèle à Dieu.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Les fils d’Ephraïm, armés de l’arc, habiles tireurs, ont tourné le dos au jour du combat!
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Ils ont répudié l’alliance de Dieu et refusé de suivre sa loi.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Ils ont oublié ses grandes œuvres et ses merveilles, dont il les avait rendus témoins.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Sous les yeux de leurs pères il accomplit des prodiges, sur la terre d’Egypte, dans les champs de Çoân.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Il fendit la mer pour leur ouvrir un passage, fit se dresser les ondes comme une digue.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Le jour, il les dirigeait au moyen de la nuée, et toute la nuit, par l’éclat du feu.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Il entrouvrit des roches dans le désert, et offrit à leur soif des flots abondants.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Il fit jaillir des torrents du granit et couler les eaux comme des fleuves.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Mais ils continuèrent à pécher contre lui, à s’insurger contre le Très-Haut dans ces régions arides.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Au fond de leur cœur, ils mirent Dieu à l’épreuve, en demandant une nourriture selon leur goût.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Ils tinrent des propos contre Dieu, disant:
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
"Dieu pourra-t-il dresser une table dans le désert? Sans doute il a frappé un rocher, et les eaux ont jailli, des torrents se sont précipités: pourra-t-il aussi donner du pain? Sera-t-il capable d’apprêter de la viande à son peuple?"
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
C’Est pourquoi l’Eternel, les ayant entendus, s’irrita; un feu s’alluma contre Jacob, et sa colère s’éleva contre Israël,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
parce qu’ils n’avaient pas eu foi en Dieu, ni témoigné de leur confiance en son secours.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Il commanda aux nuages d’en haut, et ouvrit les portes du ciel.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
Il fit pleuvoir sur eux de la manne comme nourriture, et leur octroya du blé céleste.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Tous eurent à manger de ce pain de délices: il leur avait envoyé des vivres à satiété.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Puis il abattit le vent d’Est sous les cieux, et sa puissance déchaîna le vent du Midi.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Il fit pleuvoir sur eux de la viande dru comme la poussière, des oiseaux ailés nombreux comme le sable de la mer;
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
il les fit tomber au milieu de leur camp, tout autour de leurs tentes.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Ils mangèrent et furent pleinement rassasiés: il leur accorda l’objet de leur convoitise.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Eux n’avaient pas encore assouvi leur désir, la nourriture était encore dans leur bouche,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
que la colère de Dieu s’éleva contre eux; il en décima les plus vigoureux et coucha à terre les gens d’élite en Israël.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Malgré cela ils péchèrent encore, et n’ajoutèrent point foi à ses merveilles.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Il mit donc fin à leurs jours par un souffle, à leurs années par des coups soudains.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Quand il les faisait ainsi périr, ils le recherchaient; venant à résipiscence, ils se mettaient en quête de Dieu.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Alors ils se souvenaient que Dieu était leur rocher, le Dieu suprême leur libérateur.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Ils l’amadouaient avec leur bouche, en paroles ils lui offraient des hommages menteurs,
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
mais leur cœur n’était pas de bonne foi à son égard; ils n’étaient pas sincèrement attachés à son alliance.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Mais lui, plein de miséricorde, pardonne les fautes, pour ne pas consommer des ruines; bien souvent il laisse sa colère s’apaiser, et n’a garde de déchaîner tout son courroux.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Il se souvint donc que c’étaient de faibles créatures, un souffle qui s’évanouit sans retour.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Que de fois ils s’insurgèrent contre lui dans le désert et l’offensèrent dans ces lieux solitaires!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Ils revenaient sans cesse à la charge, mettant à l’épreuve le Tout-Puissant, et défiant le Saint d’Israël.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Ils étaient oublieux de sa puissance, oublieux du jour où il les délivra de l’ennemi;
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
car il fit éclater ses prodiges en Egypte, et ses miracles dans les champs de Çoân.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
Il changea en sang leurs fleuves, et leurs cours d’eau ne furent plus potables.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Il lança contre eux des bêtes malfaisantes pour les dévorer, des grenouilles pour les ruiner.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
Il livra leurs plantations aux locustes, et le produit de leur travail aux sauterelles.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Par la grêle il fit périr leurs vignes, et leurs sycomores par les giboulées.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
Il abandonna leur bétail en proie à la grêle, et leurs troupeaux aux ravages de la foudre.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Il lâcha sur eux le feu de sa colère, courroux, malédiction et fléaux, tout un essaim d’anges malfaisants.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Il donna libre cours à sa colère, ne les préserva pas eux-mêmes de la mort, mais les fit succomber, victimes de la peste.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
Il frappa tout premier-né en Egypte, les prémices de leur vigueur dans les tentes de Cham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Il mit en marche son peuple comme des brebis, et les conduisit comme un troupeau dans le désert.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Il les fit avancer en sécurité, sans qu’ils eussent rien à craindre, alors que la mer s’était refermée sur leurs ennemis.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Il les amena sur son saint territoire, sur cette montagne acquise par sa droite.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
Il chassa des peuplades devant eux, leur en distribua le pays par lots héréditaires, et établit dans leurs tentes les tribus d’Israël.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Mais, redevenus rebelles, ils tentèrent le Dieu suprême, et cessèrent d’observer ses statuts.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Ils se dévoyèrent, devinrent infidèles comme leurs pères, se retournèrent comme un arc perfide.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Ils irritèrent Dieu par leurs hauts lieux, et, par leurs images sculptées, allumèrent sa jalousie.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Dieu entendit et s’emporta, eut un profond dégoût d’Israël.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
Il délaissa la résidence de Silo, le tabernacle qu’il avait établi parmi les hommes.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
Il laissa s’en aller en captivité sa puissance, et sa gloire tomber entre les mains de l’ennemi.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
Il livra son peuple au glaive, et s’emporta contre son héritage.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Ses jeunes gens, le feu les dévora, ses jeunes filles ne connurent aucun chant d’hyménée.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Ses prêtres tombèrent par l’épée, et ses veuves ne pleurèrent point.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Alors le Seigneur se réveilla, tel un homme qui a dormi, tel un guerrier exalté par le vin.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
Ses coups firent reculer ses adversaires: il leur infligea un opprobre éternel.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Mais il rejeta le tabernacle de Joseph, et cessa de préférer la tribu d’Ephraïm.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Il porta son choix sur la tribu de Juda, sur le mont Sion, qu’il avait pris en affection;
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
il bâtit son sanctuaire, solide comme les hauteurs célestes, comme la terre qu’il a fondée pour l’éternité.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Il élut David, son serviteur, et lui fit quitter les parcs des troupeaux.
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
Du milieu des brebis allaitant leurs petits, il l’amena pour être le pasteur de Jacob, son peuple, et d’Israël, son héritage.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Et lui, David, fut leur pasteur selon l’intégrité de son cœur, et les dirigea d’une main habile.

< Zaburi 78 >