< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
A maschil of Asaph. Hear my teaching, my people, listen to the words of my mouth.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
I will open my mouth in parables; I will sing about hidden things about the past.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
These are things that we have heard and learned, things that our ancestors have told us.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
We will not keep them from their descendants. We will tell the next generation about the praiseworthy deeds of Yahweh, his strength, and the wonders that he has done.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
For he established covenant decrees in Jacob and appointed a law in Israel. He commanded our ancestors that they were to teach them to their children.
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
He commanded this so that the generation to come might know his decrees, the children not yet born, who should tell them in turn to their own children.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
Then they would place their hope in God and not forget his deeds but keep his commandments.
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
Then they would not be like their ancestors, who were a stubborn and rebellious generation, a generation whose hearts were not right, and whose spirits were not committed and faithful to God.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
The Ephraimites were armed with bows, but they turned back on the day of battle.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
They did not keep the covenant with God, and they refused to obey his law.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
They forgot his deeds, the wonderful things that he had shown them.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
They forgot the marvelous things he did in the sight of their ancestors in the land of Egypt, in the land of Zoan.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
He divided the sea and led them across it; he made the waters to stand like walls.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
In the daytime he led them with a cloud and all the night with the light of fire.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
He split the rocks in the wilderness, and he gave them water abundantly, enough to fill the depths of the sea.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
He made streams flow out of the rock and made the water flow like rivers.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Yet they continued to sin against him, rebelling against the Most High in the wilderness.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
They challenged God in their hearts by asking for food to satisfy their appetites.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
They spoke against God; they said, “Can God really lay out a table for us in the wilderness?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
See, when he struck the rock, waters gushed out and streams overflowed. But can he give bread also? Will he provide meat for his people?”
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
When Yahweh heard this, he was angry; so his fire burned against Jacob, and his anger attacked Israel,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
because they did not believe in God and did not trust in his salvation.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Yet he commanded the skies above and opened the doors of the sky.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
He rained down manna for them to eat, and gave them the grain from heaven.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
People ate the bread of angels. He sent them food in abundance.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
He caused the east wind to blow in the sky, and by his power he guided the south wind.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
He rained down meat on them like dust, birds as numerous as the sands of the sea.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
They fell in the middle of their camp, all around their tents.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
So they ate and were full. He gave them what they craved.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
But they had not yet filled up; their food was still in their mouths.
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
Then God's anger attacked them and killed the strongest of them. He brought down the young men of Israel.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Despite this, they continued to sin and did not believe his wonderful deeds.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Therefore God cut short their days; their years were filled with terror.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Whenever God afflicted them, they would start to seek him, and they would return and look earnestly for him.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
They would call to mind that God was their rock and that the Most High God was their rescuer.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
But they would flatter him with their mouth and lie to him with their words.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
For their hearts were not firmly fixed on him, and they were not faithful to his covenant.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Yet he, being merciful, forgave their iniquity and did not destroy them. Yes, many times he held back his anger and did not stir up all his wrath.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
He called to mind that they were made of flesh, a wind that passes away and does not return.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
How often they rebelled against him in the wilderness and grieved him in the barren regions!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Again and again they challenged God and offended the Holy One of Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
They did not think about his power, how he had rescued them from the enemy
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
when he performed his terrifying signs in Egypt and his wonders in the region of Zoan.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
He turned the Egyptians' rivers to blood so that they could not drink from their streams.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
He sent swarms of flies that devoured them and frogs that overran their land.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
He gave their crops to the grasshopper and their labor to the locust.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
He destroyed their vines with hail and their sycamore trees with more hail.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
He rained hail on their cattle and hurled lightning bolts at their livestock.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
The fierceness of his anger lashed out against them. He sent wrath, fury, and trouble like agents who bring disaster.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
He leveled a path for his anger; he did not spare them from death but gave them over to the plague.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
He killed all the firstborn in Egypt, the firstborn of their strength in the tents of Ham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
He led his own people out like sheep and guided them through the wilderness like a flock.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
He led them secure and unafraid, but the sea overwhelmed their enemies.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Then he brought them to the border of his holy land, to this mountain that his right hand acquired.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
He drove out the nations from before them and assigned them their inheritance. He settled the tribes of Israel in their tents.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Yet they challenged and defied the Most High God and did not keep his solemn commands.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
They were unfaithful and acted treacherously like their fathers; they were as undependable as a faulty bow.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
For they made him angry with their high places and provoked him to jealous anger with their idols.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
When God heard this, he was angry and completely rejected Israel.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
He abandoned the sanctuary of Shiloh, the tent where he had lived among people.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
He allowed his strength to be captured and gave his glory into the enemy's hand.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
He handed his people over to the sword, and he was angry with his heritage.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Fire devoured their young men, and their young women had no wedding songs.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Their priests fell by the sword, and their widows could not weep.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Then the Lord awakened as one from sleep, like a warrior who shouts because of wine.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
He drove his adversaries back; he put them to everlasting shame.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
He rejected the tent of Joseph, and he did not chose the tribe of Ephraim.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
He chose the tribe of Judah and Mount Zion that he loved.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
He built his sanctuary like the heavens, like the earth that he has established forever.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
He chose David, his servant, and took him from the sheepfolds.
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
He took him from following the ewes with their young, and he brought him to be shepherd of Jacob, his people, and of Israel, his heritage.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
David shepherded them with the integrity of his heart, and he guided them with the skill of his hands.

< Zaburi 78 >