< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Understanding for Asaph. Attend, O my people, to my law: incline your ears to the words of my mouth.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
I will open my mouth in parables: I will utter propositions from the beginning.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
How great things have we heard and known, and our fathers have told us.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
They have not been hidden from their children, in another generation. Declaring the praises of the Lord, and his powers, and his wonders which he hath done.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
And he set up a testimony in Jacob: and made a law in Israel. How great things he commanded our fathers, that they should make the same known to their children:
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
That another generation might know them. The children that should be born and should rise up, and declare them to their children.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
That they may put their hope in God and may not forget the works of God: and may seek his commandments.
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
That they may not become like their fathers, a perverse and exasperating generation. A generation that set not their heart aright: and whose spirit was not faithful to God.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
The sons of Ephraim who bend and shoot with the bow: they have turned back in the day of battle.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
They kept not the covenant of God: and in his law they would not walk.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
And they forgot his benefits, and his wonders that he had shewn them.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Wonderful things did he do in the sight of their fathers, in the land of Egypt, in the field of Tanis.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
He divided the sea and brought them through: and he made the waters to stand as in a vessel.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
And he conducted them with a cloud by day: and all the night with a light of fire.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
He struck the rock in the wilderness: and gave them to drink, as out of the great deep.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
He brought forth water out of the rock: and made streams run down as rivers.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
And they added yet more sin against him: they provoked the most High to wrath in the place without water.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
And they tempted God in their hearts, by asking meat for their desires.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
And they spoke ill of God: they said: Can God furnish a table in the wilderness?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Because he struck the rock, and the waters gushed out, and the streams overflowed. Can he also give bread, or provide a table for his people?
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Therefore the Lord heard, and was angry: and a fire was kindled against Jacob, and wrath came up against Israel.
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
Because they believed not in God: and trusted not in his salvation.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
And he had commanded the clouds from above, and had opened the doors of heaven.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
And had rained down manna upon them to eat, and had given them the bread of heaven.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Man ate the bread of angels: he sent them provisions in abundance.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
He removed the south wind from heaven: and by his power brought in the southwest wind.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
And he rained upon them flesh as dust: and feathered fowls like as the sand of the sea.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
And they fell in the midst of their camp, round about their pavilions.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
So they did eat, and were filled exceedingly, and he gave them their desire:
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
They were not defrauded of that which they craved. As yet their meat was in their mouth:
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
And the wrath of God came upon them. And he slew the fat ones amongst them, and brought down the chosen men of Israel.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
In all these things they sinned still: and they believed not for his wondrous works.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
And their days were consumed in vanity, and their years in haste.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
When he slew them, then they sought him: and they returned, and came to him early in the morning.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
And they remembered that God was their helper: and the most high God their redeemer.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
And they loved him with their mouth: and with their tongue they lied unto him:
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
But their heart was not right with him: nor were they counted faithful in his covenant.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
But he is merciful, and will forgive their sins: and will not destroy them. And many a time did he turn away his anger: and did not kindle all his wrath.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
And he remembered that they are flesh: a wind that goeth and returneth not.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
How often did they provoke him in the desert: and move him to wrath in the place without water?
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
And they turned back and tempted God: and grieved the holy one of Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
They remembered not his hand, in the day that he redeemed them from the hand of him that afflicted them:
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
How he wrought his signs in Egypt, and his wonders in the field of Tanis.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
And he turned their rivers into blood, and their showers that they might, not drink.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
He sent amongst them divers sores of flies, which devoured them: and frogs which destroyed them.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
And he gave up their fruits to the blast, and their labours to the locust.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
And he destroyed their vineyards with hail, and their mulberry trees with hoarfrost.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
And he gave up their cattle to the hail, and their stock to the fire.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
And he sent upon them the wrath of his indignation: indignation and wrath and trouble, which he sent by evil angels.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
He made a way for a path to his anger: he spared not their souls from death, and their cattle he shut up in death.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
And he killed all the firstborn in the land of Egypt: the firstfruits of all their labour in the tabernacles of Cham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
And he took away his own people as sheep: and guided them in the wilderness like a flock.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
And he brought them out in hope, and they feared not: band the sea overwhelmed their enemies.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
And he brought them into the mountain of his sanctuary: the mountain which his right hand had purchased. And he cast out the Gentiles before them: and by lot divided to them their land by a line of distribution.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
And he made the tribes of Israel to dwell in their tabernacles.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Yet they tempted, and provoked the most high God: and they kept not his testimonies.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
And they turned away, and kept not the covenant: even like their fathers they were turned aside as a crooked bow.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
They provoked him to anger on their hills: and moved him to jealousy with their graven things.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
God heard, and despised them, and he reduced Israel exceedingly as it were to nothing.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
And he put away the tabernacle of Silo, his tabernacle where he dwelt among men.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
And he delivered their strength into captivity: and their beauty into the hands of the enemy.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
And he shut up his people under the sword: and he despised his inheritance.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Fire consumed their young men: and their maidens were not lamented.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Their priests fell by the sword: and their widows did not mourn.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
And the Lord was awaked as one out of sleep, and like a mighty man that hath been surfeited with wine.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
And he smote his enemies on the hinder parts: he put them to an everlasting reproach.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
And he rejected the tabernacle of Joseph: and chose not the tribe of Ephraim:
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
But he chose the tribe of Juda, mount Sion which he loved.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
And he built his sanctuary as of unicorns, in the land which he founded for ever.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
And he chose his servant David, and took him from the hocks of sheep: he brought him from following the ewes great with young,
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
To feed Jacob his servant, and Israel his inheritance.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
And he fed them in the innocence of his heart: and conducted them by the skillfulness of his hands.

< Zaburi 78 >