< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
The understanding of Asaph. O my people, attend to my law. Incline your ears to the words of my mouth.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
I will open my mouth in parables. I will speak about concepts that are from the beginning.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
We have heard and known such great things, as our fathers have described to us.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
These things have not been hidden from their sons in any generation: declaring the praises of the Lord, and his virtues, and the wonders that he has done.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
And he has received testimony with Jacob, and he has set a law within Israel. Such great things, he has commanded our fathers, so as to make these things known to their sons,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
so that another generation might know them, and so that the sons, who will be born and who will grow up, shall describe them to their sons.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
So then, may they put their hope in God, and may they not forget the works of God, and may they seek his commandments.
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
May they not become like their fathers, a perverse and exasperating generation: a generation that does not straighten their heart and whose spirit is not trustworthy with God.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
The sons of Ephraim, who bend and shoot the bow, have been turned back in the day of battle.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
They have not kept the covenant of God. And they were not willing to walk in his law.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
And they have been forgetful of his benefits, and of his miracle, which he revealed to them.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
He performed miracles in the sight of their fathers, in the land of Egypt, in the field of Tanis.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
He broke the sea and he led them through. And he stationed the waters, as if in a vessel.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
And he led them with a cloud by day, and with illumination by fire throughout the night.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
He broke through the rock in the wasteland, and he gave them to drink, as if from the great abyss.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
He brought forth water from the rock, and he conducted the waters, as if they were rivers.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
And yet, they continued to sin against him. In a waterless place, they provoked the Most High with resentment.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
And they tempted God in their hearts, by asking for food according to their desires.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
And they spoke badly about God. They said, “Would God be able to prepare a table in the desert?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
He struck the rock, and so waters flowed and the torrents flooded, but would even he be able to provide bread, or provide a table, for his people?”
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Therefore, the Lord heard, and he was dismayed, and a fire was kindled within Jacob, and an anger ascended into Israel.
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
For they neither put their trust in God, nor did they hope in his salvation.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
And he commanded the clouds from above, and he opened the doors of heaven.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
And he rained down manna upon them to eat, and he gave them the bread of heaven.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Man ate the bread of Angels. He sent them provisions in abundance.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
He transferred the south wind from heaven, and, in his virtue, he brought in the Southwest wind.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
And he rained down flesh upon them, as if it were dust, and feathered birds, as if they were the sand of the sea.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
And they fell down in the midst of their camp, encircling their tabernacles.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
And they ate until they were greatly satisfied, and he brought to them according to their desires.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
They were not cheated out of what they wanted. Their food was still in their mouth,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
and then the wrath of God came upon them. And he slew the fat ones among them, and he impeded the elect of Israel.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
In all these things, they continued to sin, and they were not trustworthy with his miracles.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
And their days faded away into vanity, and their years with haste.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
When he slew them, then they sought him. And they returned, and they drew near to him in the early morning.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
And they were mindful that God is their helper and that the Most High God is their redeemer.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
And they chose him with their mouth, and then they lied to him with their tongue.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
For their heart was not upright with him, nor have they been living faithfully in his covenant.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Yet he is merciful, and he will pardon their sins. And he will not destroy them. And he has abundantly turned aside his own wrath. And he did not enflame his wrath entirely.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
And he remembered that they are flesh: with a spirit that goes forth and does not return.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
How often did they provoke him in the desert and stir him to wrath in a waterless place?
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
And they turned back and tempted God, and they exasperated the Holy One of Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
They did not remember his hand, in the day that he redeemed them from the hand of the one troubling them.
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
Thus, he positioned his signs in Egypt and his wonders in the field of Tanis.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
And he turned their rivers into blood, along with their rain showers, so that they could not drink.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
He sent among them the common fly, and it devoured them, and the frog, and it scattered them.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
And he gave up their fruits to mold and their labors to the locust.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
And he slew their vineyards with hail and their mulberry trees with severe frost.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
And he delivered their cattle to the hail and their possessions to fire.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
And he sent the wrath of his indignation among them: indignation and wrath and tribulation, sent forth by evil angels.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
He made way for the path of his anger. He did not spare their souls from death. And he enclosed their beasts of burden in death.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
And he struck all the first-born in the land of Egypt: the first-fruits of all their labor in the tabernacles of Ham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
And he took away his own people like sheep, and he led them through the wilderness like a flock.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
And he led them out in hope, and they did not fear. And the sea covered their enemies.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
And he led them to the mountain of his sanctification: the mountain that his right hand had acquired. And he cast out the Gentiles before their face. And he divided their land by lot to them, with a line of distribution.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
And he caused the tribes of Israel to dwell in their tabernacles.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Yet they tempted and aggravated God Most High, and they did not keep his testaments.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
And they turned themselves aside, and they did not serve the covenant. In the same manner as their fathers, they were turned backwards, like a crooked bow.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
They impelled him to anger on their hills, and they provoked him to rivalry with their graven images.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
God listened, and he spurned them, and he reduced Israel greatly, almost to nothing.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
And he rejected the tabernacle of Shiloh, his tabernacle where he had dwelt among men.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
And he delivered their virtue into captivity, and their beauty into the hands of the enemy.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
And he enclosed his people with the sword, and he spurned his inheritance.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Fire consumed their young men, and their virgins were not lamented.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Their priests fell by the sword, and their widows did not weep.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
And the Lord was awakened, as if out of sleep, and like a powerful man impaired by wine.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
And he struck his enemies on the back. He gave them over to everlasting disgrace.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
And he rejected the tabernacle of Joseph, and he did not choose the tribe of Ephraim.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
But he chose the tribe of Judah: mount Zion, which he loved.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
And he built up his sanctuary, like a single-horned beast, in the land that he founded for all ages.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
And he chose his servant David, and he took him from the flocks of the sheep: he received him from following the ewes with their young,
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
in order to pasture Jacob his servant and Israel his inheritance.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
And he fed them with the innocence of his heart. And he led them with the understanding of his hands.

< Zaburi 78 >