< Zaburi 77 >

1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
برای سالار مغنیان بر یدوتون. مزمور آساف آواز من بسوی خداست و فریادمی کنم. آواز من بسوی خداست گوش خود را به من فرا خواهد گرفت.۱
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
در روز تنگی خود خداوند را طلب کردم. در شب، دست من دراز شده، بازکشیده نگشت و جان من تسلی نپذیرفت.۲
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
خدا را یاد می‌کنم و پریشان می‌شوم. تفکر می‌نمایم و روح من متحیر می‌گردد، سلاه.۳
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
چشمانم را بیدار می‌داشتی. بی‌تاب می‌شدم وسخن نمی توانستم گفت.۴
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
درباره ایام قدیم تفکرکرده‌ام. درباره سالهای زمانهای سلف.۵
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
سرودشبانه خود را بخاطر می‌آورم و در دل خود تفکرمی کنم و روح من تفتیش نموده است.۶
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
مگر خداتا به ابد ترک خواهد کرد و دیگر هرگز راضی نخواهد شد.۷
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
آیا رحمت او تا به ابد زایل شده است؟ و قول او باطل گردیده تا ابدالاباد؟۸
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
آیاخدا رافت را فراموش کرده؟ و رحمت های خودرا در غضب مسدود ساخته است؟ سلاه.۹
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
پس گفتم این ضعف من است. زهی سالهای دست راست حضرت اعلی!۱۰
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
کارهای خداوند را ذکرخواهم نمود زیرا کار عجیب تو را که از قدیم است به یاد خواهم آورد.۱۱
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
و در جمیع کارهای تو تامل خواهم کرد و در صنعتهای تو تفکرخواهم نمود.۱۲
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
‌ای خدا، طریق تو در قدوسیت است. کیست خدای بزرگ مثل خدا؟۱۳
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
تو خدایی هستی که کارهای عجیب می‌کنی و قوت خویش را بر قوم‌ها معروف گردانیده‌ای.۱۴
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
قوم خود را به بازوی خویش رهانیده‌ای یعنی بنی یعقوب وبنی یوسف را. سلاه.۱۵
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
آبها تو را دید، ای خداآبها تو را دیده، متزلزل شد. لجه‌ها نیز سخت مضطرب گردید.۱۶
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
ابرها آب بریخت و افلاک رعد بداد. تیرهای تو نیز به هر طرف روان گردید.۱۷
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
صدای رعد تو در گردباد بود و برقها ربع مسکون را روشن کرد. پس زمین مرتعش و متزلزل گردید.۱۸
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
طریق تو در دریاست و راههای تو درآبهای فراوان و آثار تو را نتوان دانست.۱۹
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
قوم خود را مثل گوسفندان راهنمایی نمودی، به‌دست موسی و هارون.۲۰

< Zaburi 77 >