< Zaburi 77 >
1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
Per il Capo de’ Musici. Secondo Jeduthun. Salmo di Asaf. La mia voce s’eleva a Dio, e io grido; la mia voce s’eleva a Dio, ed egli mi porge l’orecchio.
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
Nel giorno della mia distretta, io ho cercato il Signore; la mia mano è stata tesa durante la notte senza stancarsi, l’anima mia ha rifiutato d’esser consolata.
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
Io mi ricordo di Dio, e gemo; medito, e il mio spirito è abbattuto. (Sela)
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
Tu tieni desti gli occhi miei, sono turbato e non posso parlare.
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
Ripenso ai giorni antichi, agli anni da lungo tempo passati.
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
Mi ricordo de’ miei canti durante la notte, medito nel mio cuore, e lo spirito mio va investigando:
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
Il Signore ripudia egli in perpetuo? E non mostrerà egli più il suo favore?
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
E’ la sua benignità venuta meno per sempre? La sua parola ha ella cessato per ogni età?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
Iddio ha egli dimenticato d’aver pietà? Ha egli nell’ira chiuse le sue compassioni? (Sela)
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
E ho detto: La mia afflizione sta in questo, che la destra dell’Altissimo è mutata.
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
Io rievocherò la memoria delle opere dell’Eterno; sì, ricorderò le tue maraviglie antiche,
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
mediterò su tutte le opere tue, e ripenserò alle tue gesta.
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
O Dio, le tue vie son sante; qual è l’Iddio grande come Dio?
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
Tu sei l’Iddio che fai maraviglie; tu hai fatto conoscere la tua forza fra i popoli.
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
Tu hai, col tuo braccio, redento il tuo popolo, i figliuoli di Giacobbe e di Giuseppe. (Sela)
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
Le acque ti videro, o Dio; le acque ti videro e furono spaventate; anche gli abissi tremarono.
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
Le nubi versarono diluvi d’acqua; i cieli tuonarono; ed anche i tuoi strali volarono da ogni parte.
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
La voce del tuo tuono era nel turbine; i lampi illuminarono il mondo; la terra fu scossa e tremò.
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
La tua via fu in mezzo al mare, i tuoi sentieri in mezzo alle grandi acque, e le tue orme non furon riconosciute.
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
Tu conducesti il tuo popolo come un gregge, per mano di Mosè e d’Aaronne.