< Zaburi 77 >
1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
Au chef des chantres. D’après Jeduthun. Psaume d’Asaph. Ma voix s’élève à Dieu, et je crie; Ma voix s’élève à Dieu, et il m’écoutera.
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
Au jour de ma détresse, je cherche le Seigneur; La nuit, mes mains sont étendues sans se lasser; Mon âme refuse toute consolation.
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
Je me souviens de Dieu, et je gémis; Je médite, et mon esprit est abattu. (Pause)
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
Tu tiens mes paupières en éveil; Et, dans mon trouble, je ne puis parler.
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
Je pense aux jours anciens, Aux années d’autrefois.
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
Je pense à mes cantiques pendant la nuit, Je fais des réflexions au-dedans de mon cœur, Et mon esprit médite.
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
Le Seigneur rejettera-t-il pour toujours? Ne sera-t-il plus favorable?
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
Sa bonté est-elle à jamais épuisée? Sa parole est-elle anéantie pour l’éternité?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
Dieu a-t-il oublié d’avoir compassion? A-t-il, dans sa colère, retiré sa miséricorde? (Pause)
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
Je dis: Ce qui fait ma souffrance, C’est que la droite du Très-Haut n’est plus la même…
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
Je rappellerai les œuvres de l’Éternel, Car je me souviens de tes merveilles d’autrefois;
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
Je parlerai de toutes tes œuvres, Je raconterai tes hauts faits.
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
O Dieu! Tes voies sont saintes; Quel dieu est grand comme Dieu?
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
Tu es le Dieu qui fait des prodiges; Tu as manifesté parmi les peuples ta puissance.
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
Par ton bras tu as délivré ton peuple, Les fils de Jacob et de Joseph. (Pause)
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
Les eaux t’ont vu, ô Dieu! Les eaux t’ont vu, elles ont tremblé; Les abîmes se sont émus.
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
Les nuages versèrent de l’eau par torrents, Le tonnerre retentit dans les nues, Et tes flèches volèrent de toutes parts.
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
Ton tonnerre éclata dans le tourbillon, Les éclairs illuminèrent le monde; La terre s’émut et trembla.
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
Tu te frayas un chemin par la mer, Un sentier par les grandes eaux, Et tes traces ne furent plus reconnues.
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
Tu as conduit ton peuple comme un troupeau, Par la main de Moïse et d’Aaron.