< Zaburi 77 >
1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
For the leader. On Jeduthun. Of Asaph, a psalm. Loudly will I lift my cry to God, loudly to God, so he hears to me.
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
In the day of my trouble I seek the Lord; in the night I lift my hands in prayer, refusing all comfort.
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
When I think of God, I moan; when I muse, my spirit is faint. (Selah)
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
When you hold my eyes awake, and I am restless and speechless,
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
I think of the days of old, call to mind distant years.
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
I commune with my heart in the night, I muse with inquiring spirit.
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
“Will the Lord cast us off forever, will he be gracious no more?
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
Has his love vanished forever? Is his faithfulness utterly gone?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
Has God forgotten to be gracious, or in anger withheld his compassion?” (Selah)
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
Then I said, “This it is that grieves me, that the hand of the Most High has changed.”
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
I will think of the deeds of the Lord, and remember your wonders of old.
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
I will muse on all you have wrought, and meditate on your deeds.
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
Then your way, O God, was majestic: what God was great as our God?
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
You were a God who did marvels, you did show your power to the world
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
by your arm you rescued your people, the children of Jacob and Joseph. (Selah)
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
The waters saw you, O God. The waters saw you and shivered; to their depths they trembled.
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
Clouds poured torrents of water, thunder rolled in the sky, your arrows sped to and fro.
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
Loud was the roll of your thunder, lightnings lit up the world. Earth quaked and trembled.
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
In your way, Lord, through the sea, in your path through the mighty waters, your footsteps were all unseen.
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
You did guide your folk like a flock by the hand of Moses and Aaron.