< Zaburi 77 >

1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
“For the leader of the music of the Jeduthunites. A psalm of Asaph.” I call upon God; I cry aloud for help; I call upon God, that he would hear me!
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
In the day of my trouble I seek the Lord; In the night is my hand stretched forth continually; My soul refuseth to be comforted.
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
I remember God, and am disquieted; I think of him, and my spirit is overwhelmed.
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
Thou keepest mine eyelids from closing; I am distressed, so that I cannot speak!
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
I think of the days of old, —The years of ancient times.
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
I call to remembrance my songs in the night; I meditate in my heart, And my spirit inquireth:
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
Will the Lord be angry for ever? Will he be favorable no more?
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
Is his mercy utterly withdrawn for ever? Doth his promise fail from generation to generation?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
Hath God forgotten to be gracious? Hath he in anger shut up his compassion?
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
Then I say, “This is mine affliction, A change in the right hand of the Most High.”
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
I remember the deeds of Jehovah; I think of thy wonders of old.
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
I meditate on all thy works, And talk of thy doings.
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
Thy ways, O God! are holy! Who so great a god as our God?
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
Thou art a God who doest wonders; Thou hast manifested thy power among the nations.
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
With thy strong arm thou didst redeem thy people, —The sons of Jacob and Joseph.
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
The waters saw thee, O God! The waters saw thee, and feared, And the deep trembled.
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
The clouds poured out water, The skies sent forth thunder, And thine arrows flew.
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
Thy thunder roared in the whirlwind; Thy lightning illumined the world; The earth trembled and shook.
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
Thy way was through the sea, And thy path through great waters; And thy footsteps could not be found.
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
Thou didst lead thy people like a flock, By the hands of Moses and Aaron.

< Zaburi 77 >