< Zaburi 77 >

1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
For the excellent musician Ieduthun. A Psalme committed to Asaph. My voyce came to God, when I cryed: my voyce came to God, and he heard me.
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
In the day of my trouble I sought ye Lord: my sore ranne and ceased not in the night: my soule refused comfort.
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
I did thinke vpon God, and was troubled: I praied, and my spirit was full of anguish. (Selah)
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
Thou keepest mine eyes waking: I was astonied and could not speake.
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
Then I considered the daies of olde, and the yeeres of ancient time.
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
I called to remembrance my song in the night: I communed with mine owne heart, and my spirit searched diligently.
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
Will the Lord absent him selfe for euer? and will he shewe no more fauour?
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
Is his mercie cleane gone for euer? doeth his promise faile for euermore?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
Hath God forgotten to be mercifull? hath he shut vp his teder mercies in displeasure? (Selah)
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
And I sayde, This is my death: yet I remembred the yeeres of the right hand of the most High.
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
I remembred the workes of the Lord: certainely I remembred thy wonders of olde.
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
I did also meditate all thy woorkes, and did deuise of thine actes, saying,
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
Thy way, O God, is in the Sanctuarie: who is so great a God as our God!
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
Thou art ye God that doest wonders: thou hast declared thy power among the people.
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
Thou hast redeemed thy people with thine arme, euen the sonnes of Iaakob and Ioseph. (Selah)
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
The waters sawe thee, O God: the waters sawe thee, and were afraide: yea, the depths trembled.
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
The cloudes powred out water: the heauens gaue a sounde: yea, thine arrowes went abroade.
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
The voyce of thy thunder was rounde about: the lightnings lightened the worlde: the earth trembled and shooke.
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
Thy way is in the Sea, and thy paths in the great waters, and thy footesteps are not knowen.
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
Thou diddest leade thy people like sheepe by the hand of Moses and Aaron.

< Zaburi 77 >