< Zaburi 76 >

1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
ʼElohim es conocido en Judá, Y en Israel es grande su Nombre.
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
En Salén está su Tabernáculo. Su lugar de morada también está en Sion.
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
Allí quebró las flechas encendidas, El escudo y la espada y las armas de guerra. (Selah)
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
¡Eres esplendoroso! ¡Más majestuoso que las montañas de caza!
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
Los valientes fueron saqueados. Duermen su sueño. Ninguno de los soldados pudo usar sus manos.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
¡A tu reprensión, oh ʼElohim de Jacob, Tanto jinete como caballo fueron lanzados a un sueño mortal!
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
¡Tú, solo Tú debes ser temido! ¿Y quién puede permanecer en tu Presencia cuando estás airado?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
Desde los cielos hiciste oír la sentencia. La tierra tuvo temor y permaneció quieta
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
Cuando ʼElohim se levantó a juzgar, A salvar a todos los mansos de la tierra. (Selah)
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
Ciertamente las iras del hombre te exaltarán, Y te atarás con los sobrevivientes de las iras.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Hagan votos a Yavé su ʼElohim y cúmplanlos. Que todos los que lo rodean traigan presentes al que debe ser temido.
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
Él humillará el espíritu de magistrados. Él es temido por los reyes de la tierra.

< Zaburi 76 >