< Zaburi 76 >

1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
Начальнику хора. На струнных орудиях. Псалом Асафа. Песнь. Ведом в Иудее Бог; у Израиля велико имя Его.
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
И было в Салиме жилище Его и пребывание Его на Сионе.
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
Там сокрушил Он стрелы лука, щит и меч и брань.
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
Ты славен, могущественнее гор хищнических.
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
Крепкие сердцем стали добычею, уснули сном своим, и не нашли все мужи силы рук своих.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
От прещения Твоего, Боже Иакова, вздремали и колесница и конь.
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
Ты страшен, и кто устоит пред лицем Твоим во время гнева Твоего?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
С небес Ты возвестил суд; земля убоялась и утихла,
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
когда восстал Бог на суд, чтобы спасти всех угнетенных земли.
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
И гнев человеческий обратится во славу Тебе: остаток гнева Ты укротишь.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Делайте и воздавайте обеты Господу, Богу вашему; все, которые вокруг Него, да принесут дары Страшному:
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
Он укрощает дух князей, Он страшен для царей земных.

< Zaburi 76 >