< Zaburi 76 >
1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
Jusqu'à la Fin. Jusqu'à la Fin avec les hymnes, psaume d'Asaph, chant concernant les Assyriens. Dieu est connu en Judée; son nom est grand en Israël.
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
Et son lieu est dans la paix, et sa demeure est dans Sion.
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
C'est là qu'il a brisé la force des arcs, et les armures, et le glaive, et la guerre.
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
Tu éclaires merveilleusement du haut des montagnes éternelles.
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
Tous les insensés ont été troublés en leur cœur. Ils ont dormi leur sommeil, et tous les favoris de la richesse n'ont rien trouvé dans leurs mains.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
A tes approches, Dieu de Jacob, les cavaliers se sont endormis sur leurs chevaux.
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
Tu es redoutable, et qui donc résisterait à ta colère?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
Du haut du ciel tu as fait entendre ton jugement; la terre a eu peur, et s'est tenue en repos,
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
Lorsque Dieu s'est levé pour juger et pour sauver les doux en leur cœur.
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
La pensée de l'homme te rendra grâces, et le mémorial de cette pensée te fêtera.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Faites des vœux à Dieu notre Seigneur, et accomplissez-les; tous ceux qui se rassemblent autour de lui feront des offrandes au Dieu terrible,
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
A celui qui ôte l'esprit aux princes et qui est terrible aux rois de la terre.