< Zaburi 76 >

1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
For the leader. With instrumental music. A psalm of Asaph, a song. God has made himself known in Judah, his name is great in Israel.
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
His tent is in Salem, his dwelling in Zion.
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
There he broke the lightning arrows, shield, sword, and weapons of war. (Selah)
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
Terrible is your splendor on the everlasting mountains.
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
Despoiled were the stout of heart; in the sleep into which they had fallen, none of the warriors could lift a hand.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
At your rebuke, God of Jacob, sank chariot and horse to sleep.
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
Awful are you: who can stand before you, when once you are angry?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
The judgment you gave from heaven frightened the earth into silence,
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
when God arose to judgment to save the oppressed of the earth. (Selah)
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
The fiercest will praise you, to you will the remnant hold festival.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Vow and pay to Lord your God, and let all who are round him bring presents.
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
He lops off the courage of princes, and with terror fills kings of the earth.

< Zaburi 76 >