< Zaburi 75 >

1 Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
Para o regente, conforme “altachete”; salmo e cântico de Asafe: Louvamos a ti, ó Deus; louvamos, e perto [está] o teu nome; são anunciadas as tuas maravilhas.
2 Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
O que eu recebi, no [tempo] determinado, julgarei de forma justa.
3 Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
A terra e todos os seus moradores [são] dissolvidos; [porém] eu fortifiquei suas colunas. (Selá)
4 Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
Eu disse aos orgulhosos: Não sejais orgulhosos! E aos perversos: Não exalteis o vosso poder!
5 Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
Não confieis em vosso poder, nem faleis com arrogância.
6 Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
Porque a exaltação não vem do oriente, nem do ocidente, nem do deserto;
7 Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
Mas sim [de] Deus, que é o Juiz; ele abate a um, e exalta a outro.
8 Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
Porque o SENHOR [tem] um copo na mão; com vinho espumado, cheio de mistura, e ele o derramará; e os perversos da terra o beberão e sugarão até seus restos.
9 Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
Mas eu [o] anunciarei para sempre; cantarei louvores ao Deus de Jacó.
10 Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”
E cortarei todas as arrogâncias dos perversos; [mas] os rostos dos justos serão exaltados.

< Zaburi 75 >