< Zaburi 75 >

1 Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
למנצח אל-תשחת מזמור לאסף שיר ב הודינו לך אלהים--הודינו וקרוב שמך ספרו נפלאותיך
2 Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
כי אקח מועד אני מישרים אשפט
3 Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
נמגים ארץ וכל-ישביה אנכי תכנתי עמודיה סלה
4 Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
אמרתי להוללים אל-תהלו ולרשעים אל-תרימו קרן
5 Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
אל-תרימו למרום קרנכם תדברו בצואר עתק
6 Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
כי לא ממוצא וממערב ולא ממדבר הרים
7 Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
כי-אלהים שפט זה ישפיל וזה ירים
8 Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
כי כוס ביד-יהוה ויין חמר מלא מסך-- ויגר מזה אך-שמריה ימצו ישתו כל רשעי-ארץ
9 Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
ואני אגיד לעלם אזמרה לאלהי יעקב
10 Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”
וכל-קרני רשעים אגדע תרוממנה קרנות צדיק

< Zaburi 75 >