< Zaburi 75 >

1 Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
“For the leader of the music. To the tune of “Do not destroy.” A psalm of Asaph.” We give thanks to thee, O God! we give thanks to thee, and near is thy name; Men shall declare thy wondrous deeds!
2 Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
“When I see my time, Then will I judge with equity.
3 Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
The earth trembleth, and all her inhabitants; But I uphold her pillars.”
4 Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
I say to the proud, Behave not proudly! To the wicked, Lift not up your horn!
5 Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
Lift not up your horn on high, And speak not with a stiff neck!
6 Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
For promotion cometh neither from the east, nor from the west, nor from the south;
7 Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
But it is God that judgeth; He putteth down one, and setteth up another.
8 Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
For in the hand of the LORD there is a cup; The wine is foaming and full of spices, And of it he poureth out; Even to the dregs shall all the wicked of the earth drink it.
9 Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
Therefore I will extol him for ever; I will sing praise to the God of Jacob.
10 Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”
“I will bring down all the power of the wicked; But the righteous shall lift up their heads.”

< Zaburi 75 >