< Zaburi 75 >

1 Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
For the music director. A psalm of Asaph. According to “Do Not Destroy.” A song. We thank you, God, we thank you because you are close beside us. People tell about the wonderful things you have done.
2 Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
God says, “When the time I have decided comes, I will judge fairly.
3 Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
When the earth quakes, and all its inhabitants tremble, I am the one who holds it steady. (Selah)
4 Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
To those who boast I say, ‘Don't boast!’ I tell the wicked, ‘Don't be proud!’
5 Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
No, don't be proud and arrogant, insulting heaven.”
6 Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
For no one, from the east to the west, or from the wilderness, should think so highly of themselves.
7 Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
God is the one who decides—who he will bring down and who he will lift up.
8 Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
For the Lord has a cup in his hand, full of bubbling wine mixed with spices. He pours it out, and all the wicked drink it deeply, down to the last drop.
9 Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
But I will speak about you forever. I will sing praises to the God of Jacob.
10 Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”
For God says, “I will break the power of the wicked; but I will give my support to those who do what is good.”

< Zaburi 75 >