< Zaburi 75 >
1 Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
Unto the end, corrupt not, a psalm of a canticle for Asaph. We will praise thee, O God: we will praise, and we will call upon thy name. We will relate thy wondrous works:
2 Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
When I shall take a time, I will judge justices.
3 Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
The earth is melted, and all that dwell therein: I have established the pillars thereof.
4 Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
I said to the wicked: Do not act wickedly: and to the sinners: Lift not up the horn.
5 Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
Lift not up your horn on high: speak not iniquity against God.
6 Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
For neither from the east, nor from the west, nor from the desert hills:
7 Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
For God is the judge. One he putteth down, and another he lifteth up:
8 Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
For in the hand of the Lord there is a cup of strong wine full of mixture. And he hath poured it out from this to that: but the dregs thereof are not emptied: all the sinners of the earth shall drink.
9 Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
But I will declare for ever: I will sing to the God of Jacob.
10 Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”
And I will break all the horns of sinners: but the horns of the just shall be exalted.