< Zaburi 74 >

1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
Maschil di Asaf O DIO, perchè [ci] hai scacciati in perpetuo? [Perchè] fuma l'ira tua contro alla greggia del tuo pasco?
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
Ricordati della tua raunanza, [la quale] tu acquistasti anticamente; Della tribù della tua eredità [che] tu riscotesti; Del monte di Sion, nel quale tu abitasti.
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
Muovi i passi verso le ruine perpetue, [Verso] tutto il male [che] i nemici han fatto nel [luogo] santo.
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
I tuoi nemici han ruggito in mezzo del tuo Tempio; [Vi] hanno poste le loro insegne [per] segnali.
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
[Ciò] sarà noto; come chi, [levando] ad alto delle scuri, Le avventa contro a un cespo di legne;
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
Così ora hanno essi, con iscuri e martelli, Fracassati tutti quanti gl'intagli di quello.
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
Hanno messi a fuoco e fiamma i tuoi santuari, Hanno profanato il tabernacolo del tuo Nome, [gettandolo] per terra.
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
Hanno detto nel cuor loro: Prediamoli tutti quanti; Hanno arsi tutti i luoghi delle raunanze di Dio in terra.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
Noi non veggiam [più] i nostri segni; Non [vi è] più profeta, E non abbiam con noi alcuno che sappia infino a quando.
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
Infino a quando, o Dio, oltraggerà l'avversario? Il nemico dispetterà egli il tuo Nome in perpetuo?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Perchè ritiri la tua mano e la tua destra? Non lasciare ch'ella ti dimori più dentro al seno.
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
Ora Iddio già ab antico [è] il mio Re. Il quale opera salvazioni in mezzo della terra.
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
Tu, colla tua forza, spartisti il mare; Tu rompesti le teste delle balene nelle acque.
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
Tu fiaccasti i capi del leviatan, E li desti per pasto al popolo de' deserti.
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
Tu facesti scoppiar fonti e torrenti; Tu seccasti fiumi grossi.
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
Tuo [è] il giorno, tua eziandio [è] la notte; Tu hai ordinata la luna e il sole.
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
Tu hai posti tutti i termini della terra; Tu hai formata la state ed il verno.
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
Ricordati di questo: che il nemico ha oltraggiato il Signore, E che il popolo stolto ha dispettato il tuo Nome.
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
Non dare alle fiere la vita della tua tortola; Non dimenticare in perpetuo la raunanza de' tuoi poveri afflitti.
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
Riguarda al Patto, Perciocchè i luoghi tenebrosi della terra sono ripieni di ricetti di violenza.
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
Non ritornisene il misero indietro svergognato; [Fa' che] il povero afflitto e il bisognoso lodino il tuo Nome.
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
Levati, o Dio, dibatti la tua lite; Ricordati dell'oltraggio che ti è fatto tuttodì dallo stolto.
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
Non dimenticar le grida de' tuoi nemici; Lo strepito di quelli che si levano contro a te sale del continuo [al cielo].

< Zaburi 74 >