< Zaburi 74 >

1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
Hymne d'Asaph. Pourquoi, ô Dieu, rejettes-tu toujours, ta colère fume-t-elle sur le troupeau dont tu es le pasteur?
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
Aie souvenir de ton peuple que tu acquis autrefois, réclamas comme ta tribu d'héritage, de la montagne de Sion, où tu fixas ta demeure!
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
Dirige tes pas vers des ruines déjà vieilles! L'ennemi dévaste tout dans le Sanctuaire.
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
Tes adversaires rugissent au sein de tes parvis: c'est leur culte qu'ils érigent en culte.
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
On dirait des hommes qui lèvent et font retomber les haches dans l'épaisseur d'un bois.
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
Et ils en brisent déjà les sculptures, sous les cognées et les marteaux à la fois.
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
Ils mettent en feu ton Sanctuaire; sacrilèges ils renversent la demeure de ton nom.
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
Ils disent en leur cœur: « Accablons-les tous ensemble! » Ils brûlent dans le pays tous les saints lieux d'assemblée.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
Nous ne voyons plus notre culte, il n'y a plus de prophète, nous n'avons personne qui sache jusques à quand…!
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
Jusques à quand, ô Dieu, l'ennemi sera-t-il insultant? Toujours l'ennemi méprisera-t-il ton nom?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Pourquoi retires-tu ta main et ta droite? Tire-la de ton sein, et extermine!
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
Cependant Dieu est mon Roi dès les temps de jadis, opérant des délivrances dans le sein du pays.
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
Par ta puissance tu entr'ouvris la mer, tu brisas les têtes des dragons dans ses eaux.
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
Tu fracassas les têtes des Léviathans, et les livras en proie aux hôtes du désert.
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
Tu fis jaillir des sources et des torrents, tu desséchas des fleuves qui ne tarissent jamais.
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
A toi est le jour, et à toi la nuit; tu disposas les luminaires et le soleil.
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
Tu as placé toutes les bornes de la terre; l'été et l'hiver, c'est toi qui les as faits.
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
Souviens-t'en: l'ennemi outrage l'Éternel, et un peuple en délire insulte à ton nom.
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
Ne livre pas aux bêtes l'âme de ta tourterelle, et n'oublie pas pour toujours la vie de tes affligés!
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
Considère l'alliance! car les retraites du pays sont pleines de repaires de la violence.
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
Ne renvoie pas l'opprimé confus! Que l'affligé et le pauvre aient à louer ton nom!
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
Lève-toi, ô Dieu, défends ta cause! Pense aux outrages que te fait l'impie tous les jours!
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
N'oublie pas la clameur de tes ennemis, la rumeur de tes adversaires qui s'élève sans cesse.

< Zaburi 74 >