< Zaburi 74 >

1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
Cantique d’Asaph. Pourquoi, ô Dieu, nous as-tu rejetés pour toujours? Pourquoi ta colère est-elle allumée contre le troupeau de ton pâturage?
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
Souviens-toi de ton peuple que tu as acquis aux jours anciens, que tu as racheté pour être la tribu de ton héritage! Souviens-toi de ta montagne de Sion où tu faisais ta résidence,
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
porte tes pas vers ces ruines irréparables; l’ennemi a tout ravagé dans le sanctuaire.
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
Tes adversaires ont rugi au milieu de tes saints parvis; ils ont établi pour emblèmes leurs emblèmes.
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
On les a vus, pareils au bûcheron, qui lève la cognée dans une épaisse forêt.
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
Et maintenant, toutes les sculptures ensemble; ils les ont brisées à coups de hache et de marteau.
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
Ils ont livré au feu ton sanctuaire; ils ont abattu et profané la demeure de ton nom.
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
Ils disaient dans leur cœur: « Détruisons-les tous ensemble! » Ils ont brûlé dans le pays tous les lieux saints.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
Nous ne voyons plus nos signes; il n’y a plus de prophète, et personne parmi nous qui sache jusques à quand...
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
Jusques à quand, ô Dieu, l’oppresseur insultera-t-il, l’ennemi blasphémera-t-il sans cesse ton nom?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Pourquoi retires-tu ta main et ta droite? Tire-la de ton sein et détruis-les!
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
Pourtant Dieu est mon roi dès les temps anciens, lui qui a opéré tant de délivrances sur la terre.
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
C’est toi qui as divisé la mer par ta puissance, toi qui as brisé la tête des monstres dans les eaux.
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
C’est toi qui as écrasé les têtes de Léviathan, et l’as donné en pâture au peuple du désert.
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
C’est toi qui as fait jaillir la source et le torrent, toi qui as mis à sec les fleuves qui ne tarissent pas.
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
A toi est le jour, à toi est la nuit; c’est toi qui as créé la lune et le soleil.
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
C’est toi qui as fixé toutes les limites de la terre; l’été et l’hiver, c’est toi qui les as établis.
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
Souviens-toi: l’ennemi insulte Yahweh, un peuple insensé blasphème ton nom!
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
Ne livre pas aux bêtes l’âme de ta tourterelle, n’oublie pas pour toujours la vie de tes pauvres.
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
Prends garde à ton alliance! car tous les coins du pays sont pleins de repaires de violence.
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
Que l’opprimé ne s’en retourne pas confus, que le malheureux et le pauvre puissent bénir ton nom!
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
Lève-toi, ô Dieu, prends en main ta cause; souviens-toi des outrages que t’adresse chaque jour l’insensé.
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
N’oublie pas les clameurs de tes adversaires, l’insolence toujours croissante de ceux qui te haïssent.

< Zaburi 74 >