< Zaburi 74 >
1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
God, why have you abandoned/rejected us? Will you keep rejecting us forever [RHQ]? Why are you angry with us, since we are like sheep in your pasture [and you are like our shepherd]? [MET, RHQ]
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
Do not forget your people whom you chose long ago, the people whom you freed [from being slaves in Egypt] and caused to become your tribe. Do not forget Jerusalem, which was (your home/where you dwelt) [on this earth].
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
Walk along [and see] where everything has been totally ruined; our enemies have destroyed everything in the sacred temple.
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
Your enemies shouted triumphantly in this sacred place; they erected their banners [to show they had defeated us].
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
They cut down all the [engraved objects in the temple] like woodsmen cut down trees.
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
Then they smashed all the carved wood with their axes and hammers.
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
[Then] they burned your temple to the ground; they caused that place where you were worshiped to be unfit for people to worship in.
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
They said to themselves, “We will destroy the Israelis completely,” and they [also] burned down all the other places where we gathered to worship God.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
All our sacred symbols (OR, miracles) are gone; there are no prophets now/any more, and no one knows how long [this situation will continue].
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
God, how long will our enemies make fun of you [RHQ]? Will they insult you [MTY] forever [RHQ]?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Why do you refuse to help [MTY, RHQ] us? Why do you keep your hand inside your cloak [instead of using it to destroy our enemies] [RHQ]?
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
God, you have been our king [all the time] since we came out of Egypt [HYP], and you have enabled us to defeat [our enemies] in the land [of Israel].
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
By your power you caused the [Red] Sea to divide; [it was as though] you smashed the heads of the [rulers of Egypt who were like] huge sea dragons [MET].
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
[It was as though] you crushed the head of the king of Egypt [MET] and gave his body to the animals in the desert to eat.
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
You caused springs and streams to flow, and you [also] dried up rivers that had never dried up previously.
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
You created the days and the nights, and you put the sun and the moon in their places.
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
You determined where the oceans end and the land begins, and you created the summer/hot season and the winter/cold season.
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
Yahweh, do not forget that your enemies laugh at you, and that it is foolish people who despise you [MTY].
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
Do not let your helpless people [MET] fall into the hands of their cruel enemies; do not forget your suffering/persecuted people.
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
Do not forget the agreement that you made with us; remember that there are violent people in every dark place on the earth.
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
Do not allow your oppressed people to be disgraced; help those poor and needy people in order that they will [again] praise you [MTY].
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
God, arise and defend yourself [by defending your people]! Do not forget that foolish people laugh at you (all day long/continually)!
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
Do not forget that your enemies shout angrily [at you]; the uproar that they make [while they oppose you] never stops.