< Zaburi 73 >

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
Psalmus Asaph. Quam bonus Israel Deus his qui recto sunt corde!
2 Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
Mei autem pene moti sunt pedes: pene effusi sunt gressus mei.
3 kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
Quia zelavi super iniquos, pacem peccatorum videns.
4 Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
Quia non est respectus morti eorum: et firmamentum in plaga eorum.
5 Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
In labore hominum non sunt, et cum hominibus non flagellabuntur:
6 Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
Ideo tenuit eos superbia, operti sunt iniquitate et impietate sua.
7 Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
Prodiit quasi ex adipe iniquitas eorum: transierunt in affectum cordis.
8 Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
Cogitaverunt, et locuti sunt nequitiam: iniquitatem in excelso locuti sunt.
9 Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
Posuerunt in cælum os suum: et lingua eorum transivit in terra.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
Ideo convertetur populus meus hic: et dies pleni invenientur in eis.
11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
Et dixerunt: Quomodo scit Deus, et si est scientia in excelso?
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
Ecce ipsi peccatores, et abundantes in sæculo, obtinuerunt divitias.
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
Et dixi: Ergo sine causa iustificavi cor meum, et lavi inter innocentes manus meas:
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
Et fui flagellatus tota die, et castigatio mea in matutinis.
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
Si dicebam: Narrabo sic: ecce nationem filiorum tuorum reprobavi.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
Existimabam ut cognoscerem hoc, labor est ante me:
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
Donec intrem in Sanctuarium Dei: et intelligam in novissimis eorum.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
Verumtamen propter dolos posuisti eis: deiecisti eos dum allevarentur.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
Quomodo facti sunt in desolationem, subito defecerunt: perierunt propter iniquitatem suam.
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
Velut somnium surgentium Domine, in civitate tua imaginem ipsorum ad nihilum rediges.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
Quia inflammatum est cor meum, et renes mei commutati sunt:
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
et ego ad nihilum redactus sum, et nescivi.
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
Ut iumentum factus sum apud te: et ego semper tecum.
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
Tenuisti manum dexteram meam: et in voluntate tua deduxisti me, et cum gloria suscepisti me.
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
Quid enim mihi est in cælo? et a te quid volui super terram?
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
Defecit caro mea et cor meum: Deus cordis mei, et pars mea Deus in æternum.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Quia ecce, qui elongant se a te, peribunt: perdidisti omnes, qui fornicantur abs te.
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
Mihi autem adhærere Deo bonum est: ponere in Domino Deo spem meam: ut annunciem omnes prædicationes tuas, in portis filiæ Sion.

< Zaburi 73 >