< Zaburi 73 >

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
(아삽의 시) 하나님이 참으로 이스라엘 중 마음이 정결한 자에게 선을 행하시나
2 Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
나는 거의 실족할 뻔 하였고 내 걸음이 미끄러질 뻔 하였으니
3 kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
이는 내가 악인의 형통함을 보고 오만한 자를 질시하였음이로다
4 Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
저희는 죽는 때에도 고통이 없고 그 힘이 건강하며
5 Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
타인과 같은 고난이 없고 타인과 같은 재앙도 없나니
6 Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
그러므로 교만이 저희 목걸이요 강포가 저희의 입는 옷이며
7 Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
살찜으로 저희 눈이 솟아나며 저희 소득은 마음의 소원보다 지나며
8 Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
저희는 능욕하며 악하게 압제하여 말하며 거만히 말하며
9 Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
저희 입은 하늘에 두고 저희 혀는 땅에 두루 다니도다
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
그러므로 그 백성이 이리로 돌아와서 잔에 가득한 물을 다 마시며
11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
말하기를 하나님이 어찌 알랴 지극히 높은 자에게 지식이 있으랴 하도다
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
볼지어다! 이들은 악인이라 항상 평안하고 재물은 더 하도다
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
내가 내 마음을 정히 하며 내 손을 씻어 무죄하다 한 것이 실로 헛되도다
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
나는 종일 재앙을 당하며 아침마다 징책을 보았도다
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
내가 만일 스스로 이르기를 내가 이렇게 말하리라 하였더면 주의 아들들의 시대를 대하여 궤휼을 행하였으리이다
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
내가 어찌면 이를 알까 하여 생각한즉 내게 심히 곤란하더니
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
하나님의 성소에 들어갈 때에야 저희 결국을 내가 깨달았나이다
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
주께서 참으로 저희를 미끄러운 곳에 두시며 파멸에 던지시니
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
저희가 어찌 그리 졸지에 황폐되었는가 놀람으로 전멸하였나이다
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
주여, 사람이 깬 후에는 꿈을 무시함같이 주께서 깨신 후에 저희 형상을 멸시하시리이다
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
내 마음이 산란하며 내 심장이 찔렸나이다
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
내가 이같이 우매 무지하니 주의 앞에 짐승이오나
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
내가 항상 주와 함께하니 주께서 내 오른손을 붙드셨나이다
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
주의 교훈으로 나를 인도하시고 후에는 영광으로 나를 영접하시리니
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
하늘에서는 주 외에 누가 내게 있리요 땅에서는 주 밖에 나의 사모할 자 없나이다
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
내 육체와 마음은 쇠잔하나 하나님은 내 마음의 반석이시요 영원한 분깃이시라
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
대저 주를 멀리하는 자는 망하리니 음녀 같이 주를 떠난 자를 주께서 다 멸하셨나이다
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
하나님께 가까이 함이 내게 복이라 내가 주 여호와를 나의 피난처로 삼아 주의 모든 행사를 전파하리이다

< Zaburi 73 >