< Zaburi 73 >

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
A Psalme committed to Asaph. Yet God is good to Israel: euen, to the pure in heart.
2 Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
As for me, my feete were almost gone: my steps had well neere slipt.
3 kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
For I feared at the foolish, when I sawe the prosperitie of the wicked.
4 Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
For there are no bandes in their death, but they are lustie and strong.
5 Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
They are not in trouble as other men, neither are they plagued with other men.
6 Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
Therefore pride is as a chayne vnto them, and crueltie couereth them as a garment.
7 Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
Their eyes stande out for fatnesse: they haue more then heart can wish.
8 Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
They are licentious, and speake wickedly of their oppression: they talke presumptuously.
9 Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
They set their mouth against heauen, and their tongue walketh through the earth.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
Therefore his people turne hither: for waters of a full cup are wrung out to them.
11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
And they say, Howe doeth God know it? or is there knowledge in the most High?
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
Lo, these are the wicked, yet prosper they alway, and increase in riches.
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
Certainely I haue clensed mine heart in vaine, and washed mine hands in innocencie.
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
For dayly haue I bene punished, and chastened euery morning.
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
If I say, I will iudge thus, beholde the generation of thy children: I haue trespassed.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
Then thought I to know this, but it was too painefull for me,
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
Vntill I went into the Sanctuarie of God: then vnderstoode I their ende.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
Surely thou hast set them in slipperie places, and castest them downe into desolation.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
How suddenly are they destroyed, perished and horribly consumed,
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
As a dreame when one awaketh! O Lord, when thou raisest vs vp, thou shalt make their image despised.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
Certainely mine heart was vexed, and I was pricked in my reines:
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
So foolish was I and ignorant: I was a beast before thee.
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
Yet I was alway with thee: thou hast holden me by my right hand.
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
Thou wilt guide me by thy counsell, and afterward receiue me to glory.
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
Whom haue I in heauen but thee? and I haue desired none in the earth with thee.
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
My flesh fayleth and mine heart also: but God is the strength of mine heart, and my portion for euer.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For loe, they that withdrawe themselues from thee, shall perish: thou destroyest all them that goe a whoring from thee.
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
As for me, it is good for me to draw neere to God: therefore I haue put my trust in the Lord God, that I may declare all thy workes.

< Zaburi 73 >