< Zaburi 73 >
1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
A Psalm of Asaph. How good is God to Israel, to those who are upright in heart.
2 Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
But my feet were nearly moved; my steps had nearly slipped.
3 kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
For I was zealous over the iniquitous, seeing the peacefulness of sinners.
4 Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
For they have no respect for their death, nor do they have support in their wounds.
5 Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
They are not with the hardships of men, nor will they be scourged with men.
6 Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
Therefore, arrogance has held on to them. They have been covered with their iniquity and impiety.
7 Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
Their iniquity has proceeded, as if from fat. They have parted from the affection of the heart.
8 Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
They have thought and spoken wickedness. They have spoken iniquity in high places.
9 Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
They have set their mouth against heaven, and their tongue has traversed the earth.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
Therefore, my people will be converted here, and fullness of days will be found in them.
11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
And they said, “How would God know?” and, “Isn’t there knowledge in high places?”
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
Behold, these are sinners, and, abounding in this age, they have obtained riches.
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
And I said: So then, it is without purpose that I have justified my heart and washed my hands among the innocent.
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
And I have been scourged all day long, and I have received my chastisement in the mornings.
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
If I were to say that I would explain this: Behold, I would condemn this nation of your sons.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
I considered, so that I might know this. It is a hardship before me,
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
until I may enter into the Sanctuary of God, and understand it to its last part.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
So, because of deceitfulness, truly, you have placed it before them. While they were being lifted up, you were casting them down.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
How have they been brought to desolation? They have suddenly failed. They have perished because of their iniquity.
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
As a dream is to those who awaken, O Lord, so will you reduce their image to nothing in your city.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
For my heart has been inflamed, and my temperament has been changed.
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
And so, I have been reduced to nothing, and I did not know it.
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
I have become like a beast of burden to you, and I am always with you.
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
You have held my right hand. And in your will, you have conducted me, and with your glory, you have taken me up.
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
For what is there for me in heaven? And what do I wish for on earth before you?
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
My body has failed, and my heart: O God of my heart, and God my portion, into eternity.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For behold, those who put themselves far from you will perish. You have perished all those who fornicate away from you.
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
But it is good for me to adhere to God, to put my hope in the Lord God, so that I may announce all your prophecies, at the gates of the daughter of Zion.