< Zaburi 72 >

1 Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
Of Solomon - O God judgments your to [the] king give and righteousness your to [the] son of [the] king.
2 Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
He will judge people your with righteousness and poor [people] your with justice.
3 Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
They will carry mountains peace to the people and hills in righteousness.
4 Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
He will judge - [the] poor [people] of [the] people he will save [the] children of [the] needy so he may crush [the] oppressor.
5 Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
People will fear you with [the] sun and before [the] moon generation of generations.
6 Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
He will come down like rain on mown grass like copious showers dropping of [the] earth.
7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
He will flourish in days his [the] righteous and abundance of well-being [will be] until not [the] moon.
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
And may he rule from sea to sea and from [the] river to [the] ends of [the] earth.
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
Before him they will bow down desert-dwellers and enemies his dust they will lick up.
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
[the] kings of Tarshish and [the] islands tribute they will pay [the] kings of Sheba and Seba a gift they will bring near.
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
And they may bow down to him all kings all nations they will serve him.
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
For he will deliver [the] needy [who] cries for help and [the] poor and not a helper [belongs] to him.
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
He will have compassion on [the] poor and [the] needy and [the] lives of needy [people] he will save.
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
From oppression and from violence he will redeem life their and may be precious blood their in view his.
15 Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
And may he live and he may give to him some of [the] gold of Sheba and [may] someone pray for him continually all the day may someone bless him.
16 Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
May it be an abundance of grain - in the land on [the] top of [the] mountains may it wave like Lebanon fruit its and may people blossom from [the] city like [the] vegetation of the earth.
17 Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
May it be name his for ever before [the] sun (may it increase *Q(K)*) name his and may they bless themselves by him all nations may they call blessed him.
18 Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
[be] blessed - Yahweh God [the] God of Israel [who] does wonders to only him.
19 Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
And [be] blessed - [the] name of glory his for ever and may it be filled glory his all the earth amen - and amen.
20 Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu
They are finished [the] prayers of David [the] son of Jesse.

< Zaburi 72 >