< Zaburi 72 >

1 Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
Of Solomon. Give the king, O God, your own spirit of justice your spirit of right to the son of the king,
2 Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
that with right he may judge your people, and your downtrodden ones with justice.
3 Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
May the mountains bear weal for the people, and the hills yield fruits of justice.
4 Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
The weak may he help to their rights, may he save the sons of the needy and crush the oppressor in pieces.
5 Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
May he live as long as the sun, while the moon shines – for ages and ages.
6 Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
May he be like the rain on the meadow, like showers that water the earth.
7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
In his days may justice flourish, and welfare abound, till the moon be no more.
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
May he reign from ocean to ocean, from the river to the ends of the earth.
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
May his foes bow down before him, his enemies lick the dust.
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
May tribute be rendered by kings of the isles and of Tarshish; may gifts be brought by the kings of Sheba and Seba.
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
May all kings fall prostrate before him, and all nations yield him their service.
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
For he saves the poor when he cries, the helpless and the downtrodden.
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
He pities the weak and the poor, he saves the lives of the poor.
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
He redeems them from wrong and from violence, for dear is their blood in his sight.
15 Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
Long may he live; and may gold of Sheba be given him; prayer, too, be made for him ceaselessly, all the day long may men bless him.
16 Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
May the land have abundance of corn, to the tops of the hills may it wave. May the fruit thereof flourish like Lebanon, may men spring from the city like grass of the earth.
17 Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
May his name be blessed forever, may his fame endure as the sun. May all nations envy his blessedness, all tribes of the earth call him happy.
18 Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
Blest be the Lord God, Israel’s God, who alone does wonders;
19 Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
And blest be forever his glorious name. Let all the earth be filled with his glory. Amen and Amen.
20 Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu
Here end the prayers of David, son of Jesse.

< Zaburi 72 >