< Zaburi 72 >
1 Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
BY SOLOMON. O God, give Your judgments to the king, And Your righteousness to the king’s Son.
2 Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
He judges Your people with righteousness, And Your poor with judgment.
3 Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
The mountains bear peace to the people, And the heights by righteousness.
4 Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
He judges the poor of the people, Gives deliverance to the sons of the needy, And bruises the oppressor.
5 Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
They fear You with the sun, and before the moon, Generation—generations.
6 Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
He comes down as rain on mown grass, As showers—sprinkling the earth.
7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
The righteous flourish in His days, And abundance of peace until the moon is not.
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
And He rules from sea to sea, And from the river to the ends of the earth.
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
Desert-dwellers bow before Him, And His enemies lick the dust.
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
Kings of Tarshish and of the islands send back a present. Kings of Sheba and Seba bring a reward near.
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
And all kings bow themselves to Him, All nations serve Him,
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
For He delivers the needy who cries, And the poor when he has no helper,
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
He has pity on the poor and needy, And He saves the souls of the needy,
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
He redeems their soul from fraud and from violence, And their blood is precious in His eyes.
15 Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
And He lives, and the gold of Sheba [is] given to Him, And prayer is continually made for Him, All day He is continually blessed.
16 Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
There is a handful of grain in the earth, On the top of mountains, Its fruit shakes like Lebanon, And they flourish out of the city as the herb of the earth.
17 Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
His Name is for all time, Before the sun is His Name continued, And they bless themselves in Him, All nations pronounce Him blessed.
18 Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
Blessed is YHWH God, God of Israel, He alone is doing wonders,
19 Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
And blessed [is] the Name of His glory for all time, And the whole earth is filled [with] His glory. Amen and amen!
20 Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu
The prayers of David son of Jesse have been ended.