< Zaburi 72 >

1 Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
For Solomon. O God, give the king thy judgments, and thy righteousness unto the king's son.
2 Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
He will judge thy people with righteousness, and thine afflicted with judgment.
3 Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
The mountains shall bring peace to the people, and the hills, by righteousness.
4 Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
He will do justice to the afflicted of the people; he will save the children of the needy, and will break in pieces the oppressor.
5 Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
They shall fear thee as long as sun and moon endure, from generation to generation.
6 Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
He shall come down like rain on the mown grass, as showers that water the earth.
7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
In his days shall the righteous flourish, and abundance of peace till the moon be no more.
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
And he shall have dominion from sea to sea, and from the river unto the ends of the earth.
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
The dwellers in the desert shall bow before him, and his enemies shall lick the dust.
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
The kings of Tarshish and of the isles shall render presents; the kings of Sheba and Seba shall offer tribute:
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
Yea, all kings shall bow down before him; all nations shall serve him.
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
For he will deliver the needy who crieth, and the afflicted, who hath no helper;
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
He will have compassion on the poor and needy, and will save the souls of the needy:
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
He will redeem their souls from oppression and violence, and precious shall their blood be in his sight.
15 Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
And he shall live; and to him shall be given of the gold of Sheba; and prayer shall be made for him continually: all the day shall he be blessed.
16 Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
There shall be abundance of corn in the earth, upon the top of the mountains; the fruit thereof shall shake like Lebanon; and they of the city shall bloom like the herb of the earth.
17 Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
His name shall endure for ever; his name shall be continued as long as the sun: and [men] shall bless themselves in him; all nations shall call him blessed.
18 Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
Blessed be Jehovah Elohim, the God of Israel, who alone doeth wondrous things!
19 Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
And blessed be his glorious name for ever! and let the whole earth be filled with his glory! Amen, and Amen.
20 Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu
The prayers of David the son of Jesse are ended.

< Zaburi 72 >