< Zaburi 72 >

1 Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
A Psalm according to Solomon.
2 Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
Give your judgment, O God, to the king, and your justice to the king’s son, to judge your people with justice and your poor with judgment.
3 Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
Let the mountains take up peace for the people, and the hills, justice.
4 Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
He will judge the poor of the people, and he will bring salvation to the sons of the poor. And he will humble the false accuser.
5 Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
And he will remain, with the sun and before the moon, from generation to generation.
6 Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
He will descend like rain upon fleece, and like showers showering upon the earth.
7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
In his days, justice will rise like the sun, with abundance of peace, until the moon is taken away.
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
And he will rule from sea to sea and from the river to the limits of the whole world.
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
In his sight, the Ethiopians will fall prostrate, and his enemies will lick the ground.
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
The kings of Tarshish and the islands will offer gifts. The kings of Arabia and of Seba will bring gifts.
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
And all the kings of the earth shall adore him. All nations will serve him.
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
For he will free the poor from the powerful, and the poor one who has no helper.
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
He will spare the poor and the indigent, and he will bring salvation to the souls of the poor.
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
He will redeem their souls from usuries and from iniquity, and their names shall be honorable in his sight.
15 Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
And he will live, and to him will be given from the gold of Arabia, and by him they will always adore. They will bless him all day long.
16 Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
And there will be a firmament on earth, at the summits of mountains: its fruits will be extolled above Lebanon, and those of the city will flourish like the grass of the earth.
17 Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
May his name be blessed forever; may his name remain before the sun. And all the tribes of the earth will be blessed in him. All nations will magnify him.
18 Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
Blessed is the Lord, God of Israel, who alone does wondrous things.
19 Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
And blessed is the name of his majesty in eternity. And all the earth will be filled with his majesty. Amen. Amen.
20 Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu
The praises of David, the son of Jesse, have reached an end.

< Zaburi 72 >