< Zaburi 72 >

1 Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
所羅門的詩。 上帝啊,求你將判斷的權柄賜給王, 將公義賜給王的兒子。
2 Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
他要按公義審判你的民, 按公平審判你的困苦人。
3 Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
大山小山都要因公義使民得享平安。
4 Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
他必為民中的困苦人伸冤, 拯救窮乏之輩, 壓碎那欺壓人的。
5 Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
太陽還存,月亮還在, 人要敬畏你,直到萬代!
6 Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
他必降臨,像雨降在已割的草地上, 如甘霖滋潤田地。
7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
在他的日子,義人要發旺, 大有平安,好像月亮長存。
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
他要執掌權柄,從這海直到那海, 從大河直到地極。
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
住在曠野的,必在他面前下拜; 他的仇敵必要舔土。
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
他施和海島的王要進貢; 示巴和西巴的王要獻禮物。
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
諸王都要叩拜他; 萬國都要事奉他。
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
因為,窮乏人呼求的時候,他要搭救; 沒有人幫助的困苦人,他也要搭救。
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
他要憐恤貧寒和窮乏的人, 拯救窮苦人的性命。
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
他要救贖他們脫離欺壓和強暴; 他們的血在他眼中看為寶貴。
15 Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
他們要存活。 示巴的金子要奉給他; 人要常常為他禱告,終日稱頌他。
16 Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
在地的山頂上,五穀必然茂盛; 所結的穀實要響動,如黎巴嫩的樹林; 城裏的人要發旺,如地上的草。
17 Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
他的名要存到永遠, 要留傳如日之久。 人要因他蒙福; 萬國要稱他有福。
18 Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
獨行奇事的耶和華-以色列的上帝 是應當稱頌的!
19 Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
他榮耀的名也當稱頌,直到永遠。 願他的榮耀充滿全地! 阿們!阿們!
20 Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu
耶西的兒子-大衛的祈禱完畢。

< Zaburi 72 >