< Zaburi 71 >

1 Katika wewe, Yahwe, napatakimbilio salama; usiniache niaibishwe.
En toi, Yahvé, je trouve refuge. Ne me laisse jamais être déçu.
2 Uniokoe na kunifanya salama katika haki yako; geuzia sikio lako kwangu.
Délivre-moi dans ta justice, et sauve-moi. Prêtez l'oreille et sauvez-moi.
3 Uwe kwagu mwamba kwa ajili ya kimbilio salama ambako naweza kwenda siku zote; wewe umeamuru kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Sois pour moi un rocher de refuge où je puisse toujours aller. Donne l'ordre de me sauver, car tu es mon rocher et ma forteresse.
4 Uniokoe mimi, Mungu wangu, kutoka katika mkono wa asiye haki na katili.
Sauve-moi, mon Dieu, de la main des méchants, de la main de l'homme injuste et cruel.
5 Maana wewe ni tumaini langu, Bwana Yahwe. Nimekuamini wewe siku zote tangu nilipokuwa mtoto.
Car tu es mon espérance, Seigneur Yahvé, ma confiance de ma jeunesse.
6 Nimekuwa nikisaidiwa na wewe tangu tumboni; wewe ndiye yule uliyenitoa tumboni mwa mama yangu; sifa zangu zitakuhusu wewe siku zote.
J'ai compté sur toi depuis le ventre de ma mère. Tu es celui qui m'a sorti du ventre de ma mère. Je vous louerai toujours.
7 Mimi ni mfano bora kwa watu wangu; wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.
Je suis une merveille pour beaucoup, mais tu es mon fort refuge.
8 Mama yangu atajawa na sifa zako, siku zote akikuheshimu.
Ma bouche sera remplie de tes louanges, avec votre honneur toute la journée.
9 Usinitupe katika siku za miaka ya uzee wangu; usiniache wakati nguvu zangu zitakapoisha.
Ne me rejette pas dans ma vieillesse. Ne m'abandonne pas quand mes forces faiblissent.
10 Maana adui zangu wanazungumza kuhusu mimi; wale wanao fatilia uhai wangu wanapanga njama pamoja.
Car mes ennemis parlent de moi. Ceux qui veillent sur mon âme conspirent ensemble,
11 Wao husema, “Mungu amemuacha; mfuateni na mumchukue, maana hakuna yeyote awezaye kumuokoa yeye.”
disant: « Dieu l'a abandonné. Poursuivez-le et prenez-le, car personne ne le sauvera. »
12 Mungu, usiwe mbali nami; Mungu wangu, harakisha kunisaidia mimi.
Dieu, ne t'éloigne pas de moi. Mon Dieu, dépêchez-vous de m'aider.
13 Waaibishwe na kuharibiwa, wale walio adui wa uhai wangu; wavishwe laumu na kudharauliwa, wale watafutao kuniumiza.
Que mes accusateurs soient déçus et consumés. Qu'ils soient couverts d'opprobre et de mépris ceux qui veulent me nuire.
14 Lakini nitakutumainia wewe siku zote na nitakusifu wewe zaidi na zaidi.
Mais j'espère toujours, et s'ajoutera à toutes vos louanges.
15 Kinywa changu kitaongea kuhusu haki yako na wokovu wako mchana kutwa, ingawa ziwezi kuzielewa maana ni nyingi mno.
Ma bouche racontera ta justice, et de votre salut toute la journée, bien que je n'en connaisse pas toute la mesure.
16 Nitakuja na matendo yenye nguvu ya Bwana Yahwe; nitataja haki yako, yako pekee.
Je viendrai avec les actes puissants du Seigneur Yahvé. Je ferai mention de ta justice, même de la tienne seule.
17 Mungu, tangu ujana wangu wewe umenifundisha; hata sasa ninatangaza matendo yako ya ajabu.
Dieu, tu m'as enseigné dès ma jeunesse. Jusqu'à présent, j'ai déclaré tes merveilles.
18 Hakika, hata niwapo mzee na mvi kichwani, Mungu, usiniache mimi, kama ambavyo nimekuwa nikitanga nguvu yako kwa vizazi vijavyo, na uweza wako kwa yeyote ajaye.
Oui, même quand je serai vieux et que j'aurai des cheveux blancs, Dieu, ne m'abandonne pas, jusqu'à ce que je déclare ta force à la prochaine génération, ta puissance à tous ceux qui viendront.
19 Pia haki yako, Mungu, iko juu sana; wewe ambaye umefanya mambo makuu, Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Dieu, ta justice atteint aussi les cieux. Vous avez fait de grandes choses. Dieu, qui est comme toi?
20 Wewe ambaye umetuonesha sisi mateso mengi utatuhuisha tena na utatupandisha tena juu kutoka kwenye kina cha nchi.
Toi, qui nous as fait connaître de nombreuses et amères souffrances, tu me laisseras vivre. Tu nous feras remonter des profondeurs de la terre.
21 Uiongeze heshima yangu; rudi tena na unifariji.
Augmentez mon honneur et me réconforter à nouveau.
22 Nami pia nitakushukuru kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako, Mungu wangu; kwako nitaimba sifa kwa kinubi, Mtakatifu wa Israel.
Je te louerai aussi avec la harpe pour ta fidélité, mon Dieu. Je te chante des louanges avec la lyre, Saint d'Israël.
23 Midomo yangu itapiga kelele kwa sababu ya furaha wakati nikikuimbia sifa, hata kwa roho yangu, ambayo wewe umeikomboa.
Mes lèvres crient de joie! Mon âme, que tu as rachetée, te chante des louanges!
24 Ulimi wangu pia utaongea kuhusu haki yangu mchana kutwa; maana wameaibishwa na kuvurugwa, wale waliotafuta kuniumiza.
Ma langue parlera aussi de ta justice tout le jour, car ils sont déçus, et ils sont confus, qui veulent me faire du mal.

< Zaburi 71 >