< Zaburi 69 >

1 Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
Sé mi salvador, oh Dios; porque las aguas han llegado, hasta mi cuello.
2 Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
Mis pies están profundos en la tierra suave, donde no tengo donde apoyar los pies; He venido a aguas profundas, las olas están fluyendo sobre mí.
3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
Estoy cansado de mi llanto; mi garganta está ardiendo: mis ojos se desperdician esperando a mi Dios.
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
Los que me odian sin causa son más numerosos que los pelos de mi cabeza; aquellos que están en mi contra, falsamente deseando mi destrucción, son muy fuertes; Devolví lo que no me habían quitado.
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
Oh Dios, ves cuán tonto soy; y mi maldad es clara para ti.
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
Los que tienen esperanza en ti, no sean avergonzados por mí, oh Jehová Dios de los ejércitos; no sean abatidos por mí los que esperan, oh Dios de Israel.
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
Por tu amor he soportado ofensas; he sido avergonzado.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
Me he vuelto extraño para mis hermanos, y como un hombre de un país lejano para los hijos de mi madre.
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
Estoy ardiendo con pasión por tu casa; y los insultos que han dicho de ti han venido sobre mí.
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
Mi amargo llanto y mi falta de alimento se convirtieron en vergüenza.
11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
Cuando me puse la ropa de luto, dijeron mal de mí.
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
Soy motivo de admiración para los que tienen autoridad; una canción para aquellos que son dados a la bebida fuerte.
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
Pero en cuanto a mí, permíteme orar, oh Señor, en un momento cuando estés complacido; Oh Dios, dame una respuesta en tu gran misericordia, porque tu salvación es segura.
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
Llévame de las garras del lodo, para que no pueda descender a ella; déjame ser levantado de las aguas profundas.
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
No me dejes cubrir por las aguas corrientes; no permitas que las aguas profundas pasen por mi cabeza, y no me dejes encerrar en el inframundo.
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
Da una respuesta a mis palabras, oh Señor; porque tu misericordia es buena: no escondas de tu siervo tu rostro.
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
No me rechaces, porque estoy en problemas; rápidamente dame una respuesta.
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
Acércate a mi alma, para su salvación: sé mi salvador, por los que están contra mí.
19 Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
Has visto mi vergüenza, cómo se burlaban de mí y menospreciaron; mis enemigos están todos ante ti.
20 Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
Mi corazón se rompe con las ofensas, estoy lleno de dolor; Hice una búsqueda para que algunos se apiadaran de mí, pero no había nadie; No tenía quién me consolará.
21 Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
Ellos me dieron hiel por mi comida; y vino amargo para mi bebida.
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
Dejen que su mesa delante de ellos sea para su destrucción; deja que sus fiestas se conviertan en una trampa para ellos.
23 Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
Sean cegados sus ojos para que no vean; deja que sus cuerpos estén temblando para siempre.
24 Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
Deja que tu maldición venga sobre ellos; deja que el calor de tu ira los alcance.
25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
Da sus casas a la destrucción, y no haya nadie en sus tiendas.
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
Porque son crueles con aquel contra quien está vuelta tu mano; hacen amarga la pena de aquel que es herido por ti.
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
Su castigo se incremente; que no entren en tu justicia.
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
Sean quitados sus nombres del libro de los vivientes, que no se numeren con los justos.
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
Pero yo soy pobre y estoy lleno de tristeza; déjame ser levantado por tu salvación, oh Señor.
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
Alabaré el nombre de Dios con una canción; Le daré gloria por lo que ha hecho.
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
Esto será más agradable al Señor que un buey o un becerro de pleno crecimiento.
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
Los pobres lo verán y se alegrarán: ustedes que son amantes de Dios, dejen que sus corazones tengan vida.
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
Porque los oídos del Señor están abiertos a los pobres, y él piensa en sus prisioneros.
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
Dejen que los cielos y la tierra lo alaben, los mares y todo lo que se mueve en ellos.
35 Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
Porque Dios será el salvador de Sión y el edificador de las ciudades de Judá; para que pueda ser su lugar de descanso y herencia.
36 Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.
La simiente de sus siervos tomará parte en ella, y allí descansan los amantes de su nombre.

< Zaburi 69 >