< Zaburi 69 >

1 Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
in finem pro his qui commutabuntur David salvum me fac Deus quoniam intraverunt aquae usque ad animam meam
2 Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
infixus sum in limum profundi et non est substantia veni in altitudines maris et tempestas demersit me
3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
laboravi clamans raucae factae sunt fauces meae defecerunt oculi mei dum spero in Deum meum
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
multiplicati sunt super capillos capitis mei qui oderunt me gratis confortati sunt qui persecuti sunt me inimici mei iniuste quae non rapui tunc exsolvebam
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
Deus tu scis insipientiam meam et delicta mea a te non sunt abscondita
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
non erubescant in me qui expectant te Domine Domine virtutum non confundantur super me qui quaerunt te Deus Israhel
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
quoniam propter te sustinui obprobrium operuit confusio faciem meam
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
extraneus factus sum fratribus meis et peregrinus filiis matris meae
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
quoniam zelus domus tuae comedit me et obprobria exprobrantium tibi ceciderunt super me
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
et operui in ieiunio animam meam et factum est in obprobrium mihi
11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
et posui vestimentum meum cilicium et factus sum illis in parabolam
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
adversum me exercebantur qui sedebant in porta et in me psallebant qui bibebant vinum
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
ego vero orationem meam ad te Domine tempus beneplaciti Deus in multitudine misericordiae tuae exaudi me in veritate salutis tuae
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
eripe me de luto ut non infigar liberer ab his qui oderunt me et de profundis aquarum
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
non me demergat tempestas aquae neque absorbeat me profundum neque urgeat super me puteus os suum
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
exaudi me Domine quoniam benigna est misericordia tua secundum multitudinem miserationum tuarum respice me
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
et ne avertas faciem tuam a puero tuo quoniam tribulor velociter exaudi me
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
intende animae meae et libera eam propter inimicos meos eripe me
19 Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
tu scis inproperium meum et confusionem et reverentiam meam
20 Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
in conspectu tuo sunt omnes qui tribulant me inproperium expectavit cor meum et miseriam et sustinui qui simul contristaretur et non fuit et qui consolaretur et non inveni
21 Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
et dederunt in escam meam fel et in siti mea potaverunt me aceto
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
fiat mensa eorum coram ipsis in laqueum et in retributiones et in scandalum
23 Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
obscurentur oculi eorum ne videant et dorsum eorum semper incurva
24 Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
effunde super eos iram tuam et furor irae tuae conprehendat eos
25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
fiat habitatio eorum deserta et in tabernaculis eorum non sit qui inhabitet
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
quoniam quem tu percussisti persecuti sunt et super dolorem vulnerum meorum addiderunt
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
adpone iniquitatem super iniquitatem eorum et non intrent in iustitia tua
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
deleantur de libro viventium et cum iustis non scribantur
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
ego sum pauper et dolens salus tua Deus suscepit me
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
laudabo nomen Dei cum cantico magnificabo eum in laude
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
et placebit Deo super vitulum novellum cornua producentem et ungulas
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
videant pauperes et laetentur quaerite Deum et vivet anima vestra
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
quoniam exaudivit pauperes Dominus et vinctos suos non despexit
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
laudent illum caeli et terra mare et omnia reptilia in eis
35 Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
quoniam Deus salvam faciet Sion et aedificabuntur civitates Iudaeae et inhabitabunt ibi et hereditate adquirent eam
36 Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.
et semen servorum eius possidebunt eam et qui diligunt nomen eius habitabunt in ea

< Zaburi 69 >