< Zaburi 69 >

1 Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
Al maestro del coro. Su «I gigli». Di Davide. Salvami, o Dio: l'acqua mi giunge alla gola.
2 Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
Affondo nel fango e non ho sostegno; sono caduto in acque profonde e l'onda mi travolge.
3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
Sono sfinito dal gridare, riarse sono le mie fauci; i miei occhi si consumano nell'attesa del mio Dio.
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
Più numerosi dei capelli del mio capo sono coloro che mi odiano senza ragione. Sono potenti i nemici che mi calunniano: quanto non ho rubato, lo dovrei restituire?
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
Dio, tu conosci la mia stoltezza e le mie colpe non ti sono nascoste.
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
Chi spera in te, a causa mia non sia confuso, Signore, Dio degli eserciti; per me non si vergogni chi ti cerca, Dio d'Israele.
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
Per te io sopporto l'insulto e la vergogna mi copre la faccia;
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
sono un estraneo per i miei fratelli, un forestiero per i figli di mia madre.
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
Poiché mi divora lo zelo per la tua casa, ricadono su di me gli oltraggi di chi ti insulta.
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
Mi sono estenuato nel digiuno ed è stata per me un'infamia.
11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
Ho indossato come vestito un sacco e sono diventato il loro scherno.
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
Sparlavano di me quanti sedevano alla porta, gli ubriachi mi dileggiavano.
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
Ma io innalzo a te la mia preghiera, Signore, nel tempo della benevolenza; per la grandezza della tua bontà, rispondimi, per la fedeltà della tua salvezza, o Dio.
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
Salvami dal fango, che io non affondi, liberami dai miei nemici e dalle acque profonde.
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
Non mi sommergano i flutti delle acque e il vortice non mi travolga, l'abisso non chiuda su di me la sua bocca.
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
Rispondimi, Signore, benefica è la tua grazia; volgiti a me nella tua grande tenerezza.
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
Non nascondere il volto al tuo servo, sono in pericolo: presto, rispondimi.
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
Avvicinati a me, riscattami, salvami dai miei nemici.
19 Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
Tu conosci la mia infamia, la mia vergogna e il mio disonore; davanti a te sono tutti i miei nemici.
20 Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
L'insulto ha spezzato il mio cuore e vengo meno. Ho atteso compassione, ma invano, consolatori, ma non ne ho trovati.
21 Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
Hanno messo nel mio cibo veleno e quando avevo sete mi hanno dato aceto.
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
La loro tavola sia per essi un laccio, una insidia i loro banchetti.
23 Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
Si offuschino i loro occhi, non vedano; sfibra per sempre i loro fianchi.
24 Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
Riversa su di loro il tuo sdegno, li raggiunga la tua ira ardente.
25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
La loro casa sia desolata, senza abitanti la loro tenda;
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
perché inseguono colui che hai percosso, aggiungono dolore a chi tu hai ferito.
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
Imputa loro colpa su colpa e non ottengano la tua giustizia.
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
Siano cancellati dal libro dei viventi e tra i giusti non siano iscritti.
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
Io sono infelice e sofferente; la tua salvezza, Dio, mi ponga al sicuro.
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
Loderò il nome di Dio con il canto, lo esalterò con azioni di grazie,
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
che il Signore gradirà più dei tori, più dei giovenchi con corna e unghie.
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
Vedano gli umili e si rallegrino; si ravvivi il cuore di chi cerca Dio,
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
poiché il Signore ascolta i poveri e non disprezza i suoi che sono prigionieri.
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
A lui acclamino i cieli e la terra, i mari e quanto in essi si muove.
35 Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
Perché Dio salverà Sion, ricostruirà le città di Giuda: vi abiteranno e ne avranno il possesso.
36 Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.
La stirpe dei suoi servi ne sarà erede, e chi ama il suo nome vi porrà dimora.

< Zaburi 69 >