< Zaburi 69 >
1 Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
Au chef des chantres. Sur les lis. De David. Sauve-moi, ô Dieu! Car les eaux menacent ma vie.
2 Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
J’enfonce dans la boue, sans pouvoir me tenir; Je suis tombé dans un gouffre, et les eaux m’inondent.
3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
Je m’épuise à crier, mon gosier se dessèche, Mes yeux se consument, tandis que je regarde vers mon Dieu.
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
Ils sont plus nombreux que les cheveux de ma tête, Ceux qui me haïssent sans cause; Ils sont puissants, ceux qui veulent me perdre, Qui sont à tort mes ennemis. Ce que je n’ai pas dérobé, il faut que je le restitue.
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
O Dieu! Tu connais ma folie, Et mes fautes ne te sont point cachées.
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
Que ceux qui espèrent en toi ne soient pas confus à cause de moi, Seigneur, Éternel des armées! Que ceux qui te cherchent ne soient pas dans la honte à cause de moi, Dieu d’Israël!
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
Car c’est pour toi que je porte l’opprobre, Que la honte couvre mon visage;
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
Je suis devenu un étranger pour mes frères, Un inconnu pour les fils de ma mère.
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
Car le zèle de ta maison me dévore, Et les outrages de ceux qui t’insultent tombent sur moi.
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
Je verse des larmes et je jeûne, Et c’est ce qui m’attire l’opprobre;
11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
Je prends un sac pour vêtement, Et je suis l’objet de leurs sarcasmes.
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
Ceux qui sont assis à la porte parlent de moi, Et les buveurs de liqueurs fortes me mettent en chansons.
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
Mais je t’adresse ma prière, ô Éternel! Que ce soit le temps favorable, ô Dieu, par ta grande bonté! Réponds-moi, en m’assurant ton secours!
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
Retire-moi de la boue, et que je n’enfonce plus! Que je sois délivré de mes ennemis et du gouffre!
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
Que les flots ne m’inondent plus, Que l’abîme ne m’engloutisse pas, Et que la fosse ne se ferme pas sur moi!
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
Exauce-moi, Éternel! Car ta bonté est immense. Dans tes grandes compassions, tourne vers moi les regards,
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
Et ne cache pas ta face à ton serviteur! Puisque je suis dans la détresse, hâte-toi de m’exaucer!
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
Approche-toi de mon âme, délivre-la! Sauve-moi, à cause de mes ennemis!
19 Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
Tu connais mon opprobre, ma honte, mon ignominie; Tous mes adversaires sont devant toi.
20 Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
L’opprobre me brise le cœur, et je suis malade; J’attends de la pitié, mais en vain, Des consolateurs, et je n’en trouve aucun.
21 Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
Ils mettent du fiel dans ma nourriture, Et, pour apaiser ma soif, ils m’abreuvent de vinaigre.
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
Que leur table soit pour eux un piège, Et un filet au sein de leur sécurité!
23 Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
Que leurs yeux s’obscurcissent et ne voient plus, Et fais continuellement chanceler leurs reins!
24 Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
Répands sur eux ta colère, Et que ton ardente fureur les atteigne!
25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
Que leur demeure soit dévastée, Qu’il n’y ait plus d’habitants dans leurs tentes!
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
Car ils persécutent celui que tu frappes, Ils racontent les souffrances de ceux que tu blesses.
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
Ajoute des iniquités à leurs iniquités, Et qu’ils n’aient point part à ta miséricorde!
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
Qu’ils soient effacés du livre de vie, Et qu’ils ne soient point inscrits avec les justes!
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
Moi, je suis malheureux et souffrant: O Dieu, que ton secours me relève!
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
Je célébrerai le nom de Dieu par des cantiques, Je l’exalterai par des louanges.
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
Cela est agréable à l’Éternel, plus qu’un taureau Avec des cornes et des sabots.
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
Les malheureux le voient et se réjouissent; Vous qui cherchez Dieu, que votre cœur vive!
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
Car l’Éternel écoute les pauvres, Et il ne méprise point ses captifs.
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
Que les cieux et la terre le célèbrent, Les mers et tout ce qui s’y meut!
35 Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
Car Dieu sauvera Sion, et bâtira les villes de Juda; On s’y établira, et l’on en prendra possession;
36 Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.
La postérité de ses serviteurs en fera son héritage, Et ceux qui aiment son nom y auront leur demeure.