< Zaburi 69 >
1 Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
For the choirmaster. To the tune of “Lilies.” Of David. Save me, O God, for the waters are up to my neck.
2 Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
I have sunk into the miry depths, where there is no footing; I have drifted into deep waters, where the flood engulfs me.
3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
I am weary from my crying; my throat is parched. My eyes fail, looking for my God.
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
Those who hate me without cause outnumber the hairs of my head; many are those who would destroy me— my enemies for no reason. Though I did not steal, I must repay.
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
You know my folly, O God, and my guilt is not hidden from You.
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
May those who hope in You not be ashamed through me, O Lord GOD of Hosts; may those who seek You not be dishonored through me, O God of Israel.
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
For I have endured scorn for Your sake, and shame has covered my face.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
I have become a stranger to my brothers and a foreigner to my mother’s sons,
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
because zeal for Your house has consumed me, and the insults of those who insult You have fallen on me.
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
I wept and fasted, but it brought me reproach.
11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
I made sackcloth my clothing, and I was sport to them.
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
Those who sit at the gate mock me, and I am the song of drunkards.
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
But my prayer to You, O LORD, is for a time of favor. In Your abundant loving devotion, O God, answer me with Your sure salvation.
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
Rescue me from the mire and do not let me sink; deliver me from my foes and out of the deep waters.
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
Do not let the floods engulf me or the depths swallow me up; let not the Pit close its mouth over me.
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
Answer me, O LORD, for Your loving devotion is good; turn to me in keeping with Your great compassion.
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
Hide not Your face from Your servant, for I am in distress. Answer me quickly!
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
Draw near to my soul and redeem me; ransom me because of my foes.
19 Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
You know my reproach, my shame and disgrace. All my adversaries are before You.
20 Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
Insults have broken my heart, and I am in despair. I looked for sympathy, but there was none, for comforters, but I found no one.
21 Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
They poisoned my food with gall and gave me vinegar to quench my thirst.
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
May their table become a snare; may it be a retribution and a trap.
23 Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
May their eyes be darkened so they cannot see, and their backs be bent forever.
24 Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
Pour out Your wrath upon them, and let Your burning anger overtake them.
25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
May their place be deserted; let there be no one to dwell in their tents.
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
For they persecute the one You struck and recount the pain of those You wounded.
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
Add iniquity to their iniquity; let them not share in Your righteousness.
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
May they be blotted out of the Book of Life and not listed with the righteous.
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
But I am in pain and distress; let Your salvation protect me, O God.
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
I will praise God’s name in song and exalt Him with thanksgiving.
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
And this will please the LORD more than an ox, more than a bull with horns and hooves.
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
The humble will see and rejoice. You who seek God, let your hearts be revived!
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
For the LORD listens to the needy and does not despise His captive people.
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
Let heaven and earth praise Him, the seas and everything that moves in them.
35 Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
For God will save Zion and rebuild the cities of Judah, that they may dwell there and possess it.
36 Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.
The descendants of His servants will inherit it, and those who love His name will settle in it.