< Zaburi 68 >

1 Mungu ainuke, maadui zake watawanyike; pia wale wamchukiao wakimbie mbele zake.
TO THE OVERSEER. A PSALM. A SONG OF DAVID. God rises [and] His enemies are scattered! And those hating Him flee from His face.
2 Kama moshi uondoshwavyo, hivyo uwaondoshe wao; kama nta iyeyukavo mbele ya moto, hivyo waovu waangamizwe uweponi mwa Mungu.
You drive them away as the driving away of smoke, As the melting of wax before fire, The wicked perish at the presence of God.
3 Bali wenye haki wafurahi; washangilie mbele za Mungu; washangilie na kufurahi.
And the righteous rejoice, they exult before God, And they rejoice with gladness.
4 Mwimbieni Mungu! Lisifuni jina lake! Msifuni yule aendeshaye farasi kwenye tambarare ya bonde la Mto Yordani! Yahwe ni jina lake! Shangilieni mbele zake!
Sing to God—praise His Name, Raise up a highway for Him who is riding in deserts, In YAH [is] His Name, and exult before Him.
5 Baba wa yatima, na mwamuzi wa wajane, ni Mungu anayeishi mahali patakatifu.
Father of the fatherless, and judge of the widows, [Is] God in His holy habitation.
6 Mungu huwaweka wakiwa katika familia; yeye huwafungua wafungwa kwa kuimba bali waasi huishi katika ardhi kavu.
God—causing the lonely to dwell at home, Bringing out bound ones into prosperity, Only—the stubborn have inhabited a dry place.
7 Mungu, wewe ulipoenda mbele ya watu wako, ulipotembea kupitia jangwani, (Selah)
O God, in Your going forth before Your people, In Your stepping through the wilderness, (Selah)
8 nchi ilitetemeka; mbingu pia zilidondosha mvua katika uwepo wa Mungu, uweponi mwa Mungu wakati alipokuja Sinai, uweponi mwa Mungu, Mungu wa Israeli.
The earth has shaken, Indeed, the heavens have dropped before God, This Sinai—before God, the God of Israel.
9 Wewe, Mungu, ulituma mvua nyingi; uliuimarisha urithi wako wakati ulipokuwa umechoka.
You shake out a shower of free-will gifts, O God. Your inheritance, when it has been weary, You have established it.
10 Watu wako waliishi humo; Wewe, Mungu, uliutoa kwa wema wako kwa maskini.
Your creature has dwelt in it, You prepare for the poor in Your goodness, O God.
11 Bwana alitoa amri, na wale walio zitangaza walikuwa ni jeshi kuu.
The Lord gives the saying, The female proclaimers [are] a numerous host.
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia, na wanawake wakisubiri nyumbani kuvigawana wao na familia zao vilivyotekwa nyara.
Kings of hosts utterly flee away, And a female inhabitant of the house apportions spoil.
13 Njiwa walio vikwa fedha wakiwa na mabawa ya njano ya dhahabu. Wakati baadhi ya watu wakikaa kati ya mifugo ya kondoo, kwa nini umefanya haya?
Though you lie between two boundaries, Wings of a dove covered with silver, And her pinions with yellow gold.
14 Mwenyezi Mungu aliwatawanya Wafalme huko, ilikuwa kama vile wakati wa theluji juu ya Mlima Salmoni.
When the Mighty spreads kings in it, it snows in Salmon.
15 Mlima mkubwa ni milima wa mji wa Bashani; mlima mrefu ni mlima wa mji wa Bashani.
A hill of God [is] the hill of Bashan, A hill of heights [is] the hill of Bashan.
16 Ewe mlima mrefu wa nchi, kwa nini unatazama kwa jicho la husuda, kwenye mlima ambao Mungu ameutaka kwa ajili ya mahali ambapo yeye ataishi? Hakika, Yahwe ataishi humo milele.
Why do you envy, O high hills, The hill God has desired for His seat? YHWH also dwells forever.
17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu juu ya maelfu; Bwana yu kati yao katika mahari patakatifu, kama katika Sinai.
The chariots of God [are] myriads, thousands of changes, The Lord [is] among them, in Sinai, in the sanctuary.
18 Wewe umepaa juu; uliwaongoza mateka; umepokea zawadi kutoka kati ya watu, hata kutoka kwa wale waliopigana dhidi yako, ili kwamba wewe, Yahwe Mungu, uweze kuishi huko.
You have ascended on high, You have taken captivity captive, You have taken gifts for men, That even the stubborn may rest, O YAH God.
19 Abarikiwe Bwana, atubebeaye mizigo yetu, Mungu ambaye ni wokovu wetu. (Selah)
Blessed [is] the Lord, day by day He lays on us. God Himself [is] our salvation. (Selah)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye; Yahwe Bwana ni yule awezaye kutuokoa sisi dhidi ya kifo.
God Himself [is] to us a God for deliverances, And YHWH Lord has the outgoings of death.
21 Lakini Bwana atapiga vichwa vya adui zake, mpaka kwenye ngozi ya kichwa yenye nywele ya wale watembeao katika makosa dhidi yake.
Only—God strikes The head of His enemies, The hairy crown of a habitual walker in his guilt.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha adui zangu kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka katika kina cha bahari
The Lord said: “From Bashan I bring back, I bring back from the depths of the sea.
23 ili kwamba upate kuwaangamiza adui zako, ukichovya mguu wako katika damu, na ili kwamba ndimi za mbwa wako zipate mlo wao kutoka kwa adui zenu.”
So that you dash your foot In the blood of enemies—the tongue of Your dogs.”
24 Mungu, wameona maandamano yako, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, kwenye mahali patakatifu.
They have seen Your goings, O God, Goings of my God, my king, in the sanctuary.
25 Waimbaji walitangulia, walifuatiwa na wapiga muziki, na katikati walikuwa wanawali wakicheza ngoma.
Singers have been before, Behind [are] players on instruments, Virgins playing with timbrels in the midst.
26 Mtukuzeni Mungu katika kusanyiko; msifuni Yahwe, ninyi ukoo wa kweli wa Israeli.
In assemblies bless God, The Lord—from the fountain of Israel.
27 Kuna Benjamini kwanza, kabila dogo, kisha viongozi wa Yuda na watu wao, viongozi wa Zabuloni na viongozi wa Naftali.
There [is] little Benjamin, their ruler, Heads of Judah their defense, Heads of Zebulun—heads of Naphtali.
28 Mungu wenu, Israeli, ameamuru nguvu zenu; uzifunue kwetu nguvu zako, Mungu, kama ulivyo zifunua wakati uliopita.
Your God has commanded your strength, Be strong, O God, You have worked this for us.
29 Uzifunue nguvu zako kwetu toka katika hekalu la Yerusalemu, ambako wafalme huleta zawadi kwako.
Because of Your temple at Jerusalem, Kings bring a present to You.
30 Pigeni kelele katika vita dhidi ya wanyama wa porini katika mianzi, dhidi ya watu, lile kundi la mafahari na ndama. Wafedhehesheni na kuwalazimisha wawaletee zawadi; watawanyeni watu wapendao kupigana vita.
Rebuke a beast of the reeds, a herd of bulls, With calves of the peoples, Each humbling himself with pieces of silver, You scatter peoples delighting in conflicts.
31 Wakuu watatoka katika Misri; Ethiopia itafanya haraka kuufikisha mkono wake kwa Mungu.
Fat ones come out of Egypt, Cush causes her hands to run to God.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za nchi; (Selah) mwimbieni sifa Yahwe.
Kingdoms of the earth, sing to God, Praise the Lord! (Selah)
33 Kwake yeye apitaye juu ya mbingu za mbingu, zilizokuwepo tangu zama za kale; tazama, yeye hupiga kelele kwa nguvu
To Him who is riding on the heavens of the heavens of old, Behold, He gives with His voice a strong voice.
34 Tangazeni kuwa Mungu ni mwenye nguvu; enzi yake iko juu ya Israeli, na nguvu zake ziko angani.
Ascribe strength to God, His excellence [is] over Israel, and His strength in the clouds.
35 Mungu, mahali pako patakatifu panatisha; Mungu wa Israeli, yeye huwapa watu wake nguvu na uweza. Atukuzwe Mungu.
Fearful, O God, out of Your sanctuaries, The God of Israel Himself, Giving strength and might to the people. Blessed [is] God!

< Zaburi 68 >