< Zaburi 68 >

1 Mungu ainuke, maadui zake watawanyike; pia wale wamchukiao wakimbie mbele zake.
For the end, a Psalm of a Song by David. Let God arise, and let his enemies be scattered; and let them that hate him flee from before him.
2 Kama moshi uondoshwavyo, hivyo uwaondoshe wao; kama nta iyeyukavo mbele ya moto, hivyo waovu waangamizwe uweponi mwa Mungu.
As smoke vanishes, let them vanish: as wax melts before the fire, so let the sinners perish from before God.
3 Bali wenye haki wafurahi; washangilie mbele za Mungu; washangilie na kufurahi.
But let the righteous rejoice; let them exult before God: let them be delighted with joy.
4 Mwimbieni Mungu! Lisifuni jina lake! Msifuni yule aendeshaye farasi kwenye tambarare ya bonde la Mto Yordani! Yahwe ni jina lake! Shangilieni mbele zake!
Sing to God, sing praises to his name: make a way for him that rides upon the west (the Lord is his name) and exult before him. They shall be troubled before the face of him,
5 Baba wa yatima, na mwamuzi wa wajane, ni Mungu anayeishi mahali patakatifu.
[who is] the father of the orphans, and judge of the widows: [such is] God in his holy place.
6 Mungu huwaweka wakiwa katika familia; yeye huwafungua wafungwa kwa kuimba bali waasi huishi katika ardhi kavu.
God settles the solitary in a house; leading forth prisoners mightily, also them that act provokingly, [even] them that dwell in tombs.
7 Mungu, wewe ulipoenda mbele ya watu wako, ulipotembea kupitia jangwani, (Selah)
O God, when thou wentest forth before thy people, when thou wentest through the wilderness; (Pause)
8 nchi ilitetemeka; mbingu pia zilidondosha mvua katika uwepo wa Mungu, uweponi mwa Mungu wakati alipokuja Sinai, uweponi mwa Mungu, Mungu wa Israeli.
the earth quaked, yea, the heavens dropped [water] at the presence of the God of Sina, at the presence of the God of Israel.
9 Wewe, Mungu, ulituma mvua nyingi; uliuimarisha urithi wako wakati ulipokuwa umechoka.
O God, thou wilt grant to thine inheritance a gracious rain; for it was weary, but thou didst refresh it.
10 Watu wako waliishi humo; Wewe, Mungu, uliutoa kwa wema wako kwa maskini.
Thy creatures dwell in it: thou hast in thy goodness prepared for the poor.
11 Bwana alitoa amri, na wale walio zitangaza walikuwa ni jeshi kuu.
The Lord God will give a word to them that preach [it] in a great company.
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia, na wanawake wakisubiri nyumbani kuvigawana wao na familia zao vilivyotekwa nyara.
The king of the forces of the beloved, of the beloved, [will] even [grant them] for the beauty of the house to divide the spoils.
13 Njiwa walio vikwa fedha wakiwa na mabawa ya njano ya dhahabu. Wakati baadhi ya watu wakikaa kati ya mifugo ya kondoo, kwa nini umefanya haya?
Even if ye should lie among the lots, [ye shall have] the wings of a dove covered with silver, and her breast with yellow gold.
14 Mwenyezi Mungu aliwatawanya Wafalme huko, ilikuwa kama vile wakati wa theluji juu ya Mlima Salmoni.
When the heavenly One scatters kings upon it, they shall be made snow-white in Selmon.
15 Mlima mkubwa ni milima wa mji wa Bashani; mlima mrefu ni mlima wa mji wa Bashani.
The mountain of God is a rich mountain; a swelling mountain, a rich mountain.
16 Ewe mlima mrefu wa nchi, kwa nini unatazama kwa jicho la husuda, kwenye mlima ambao Mungu ameutaka kwa ajili ya mahali ambapo yeye ataishi? Hakika, Yahwe ataishi humo milele.
Wherefore do ye conceive [evil], ye swelling mountains? [this is] the mountain which God has delighted to dwell in; yea, the Lord will dwell [in it] for ever.
17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu juu ya maelfu; Bwana yu kati yao katika mahari patakatifu, kama katika Sinai.
The chariots of God are ten thousand fold, thousands of rejoicing ones: the Lord is among them, in Sina, in the holy place.
18 Wewe umepaa juu; uliwaongoza mateka; umepokea zawadi kutoka kati ya watu, hata kutoka kwa wale waliopigana dhidi yako, ili kwamba wewe, Yahwe Mungu, uweze kuishi huko.
Thou art gone up on high, thou hast led captivity captive, thou hast received gifts for man, yea, for [they were] rebellious, that thou mightest dwell among them.
19 Abarikiwe Bwana, atubebeaye mizigo yetu, Mungu ambaye ni wokovu wetu. (Selah)
Blessed be the Lord God, blessed be the Lord daily; and the God of our salvation shall prosper us. (Pause)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye; Yahwe Bwana ni yule awezaye kutuokoa sisi dhidi ya kifo.
Our God is the God of salvation; and to the Lord belong the issues from death.
21 Lakini Bwana atapiga vichwa vya adui zake, mpaka kwenye ngozi ya kichwa yenye nywele ya wale watembeao katika makosa dhidi yake.
But God shall crust the heads of his enemies; the hairy crown of them that go on in their trespasses.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha adui zangu kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka katika kina cha bahari
The Lord said, I will bring again from Basan, I will bring [my people] again through the depths of the sea.
23 ili kwamba upate kuwaangamiza adui zako, ukichovya mguu wako katika damu, na ili kwamba ndimi za mbwa wako zipate mlo wao kutoka kwa adui zenu.”
That thy foot may be dipped in blood, [and] the tongue of thy dogs [be stained] with that of [thine] enemies.
24 Mungu, wameona maandamano yako, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, kwenye mahali patakatifu.
Thy goings, O God, have been seen; the goings of my God, the king, in the sanctuary.
25 Waimbaji walitangulia, walifuatiwa na wapiga muziki, na katikati walikuwa wanawali wakicheza ngoma.
The princes went first, next before the players on instruments, in the midst of damsels playing on timbrels.
26 Mtukuzeni Mungu katika kusanyiko; msifuni Yahwe, ninyi ukoo wa kweli wa Israeli.
Praise God in the congregations, the Lord from the fountains of Israel.
27 Kuna Benjamini kwanza, kabila dogo, kisha viongozi wa Yuda na watu wao, viongozi wa Zabuloni na viongozi wa Naftali.
There is Benjamin the younger [one] in ecstasy, the princes of Juda their rulers, the princes of Zabulon, the princes of Nephthali.
28 Mungu wenu, Israeli, ameamuru nguvu zenu; uzifunue kwetu nguvu zako, Mungu, kama ulivyo zifunua wakati uliopita.
O God, command thou thy strength: strengthen, O God, this which thou hast wrought in us.
29 Uzifunue nguvu zako kwetu toka katika hekalu la Yerusalemu, ambako wafalme huleta zawadi kwako.
Because of thy temple at Jerusalem shall kings bring presents to thee.
30 Pigeni kelele katika vita dhidi ya wanyama wa porini katika mianzi, dhidi ya watu, lile kundi la mafahari na ndama. Wafedhehesheni na kuwalazimisha wawaletee zawadi; watawanyeni watu wapendao kupigana vita.
Rebuke the wild beasts of the reed: let the crowd of bulls with the heifers of the nations [be rebuked], so that they who have been proved with silver may not be shut out: scatter thou the nations that wish for wars.
31 Wakuu watatoka katika Misri; Ethiopia itafanya haraka kuufikisha mkono wake kwa Mungu.
Ambassadors shall arrive out of Egypt; Ethiopia shall hasten [to stretch out] her hand readily to God.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za nchi; (Selah) mwimbieni sifa Yahwe.
Sing to God, ye kingdoms of the earth; sing psalms to the Lord. (Pause)
33 Kwake yeye apitaye juu ya mbingu za mbingu, zilizokuwepo tangu zama za kale; tazama, yeye hupiga kelele kwa nguvu
Sing to God that rides on the heaven of heaven, eastward: lo, he will utter a mighty sound with his voice.
34 Tangazeni kuwa Mungu ni mwenye nguvu; enzi yake iko juu ya Israeli, na nguvu zake ziko angani.
Give ye glory to God: his excellency is over Israel, and his power is in the clouds.
35 Mungu, mahali pako patakatifu panatisha; Mungu wa Israeli, yeye huwapa watu wake nguvu na uweza. Atukuzwe Mungu.
God is wonderful in his holy [places], the God of Israel: he will give power and strength to his people: blessed be God.

< Zaburi 68 >