< Zaburi 66 >

1 Mpigieni Mungu kelele za shangwe, nchi yote;
למנצח שיר מזמור הריעו לאלהים כל הארץ׃
2 Imbeni utukufu wa jina lake; mzitukuze sifa zake.
זמרו כבוד שמו שימו כבוד תהלתו׃
3 Mwambieni Mugu, “Matendo yako yanatisha kama nini! Kwa ukuu wa nguvu zako maadui zako watajisalimisha kwako.
אמרו לאלהים מה נורא מעשיך ברב עזך יכחשו לך איביך׃
4 Nchi yote watakuabudu wewe na watakuimbia wewe; wataliimbia jina lako.” (Selah)
כל הארץ ישתחוו לך ויזמרו לך יזמרו שמך סלה׃
5 Njoni na mtazame kazi za Mungu; yeye anatisha katika matendo yake awatendeayo wanadamu.
לכו וראו מפעלות אלהים נורא עלילה על בני אדם׃
6 Aligeuza bahari kuwa nchi kavu; wao walitembea kwa mguu juu ya mto; huko tulishangilia katika yeye.
הפך ים ליבשה בנהר יעברו ברגל שם נשמחה בו׃
7 Yeye anatawala milele kwa nguvu zake; macho yake yanachunguza mataifa; waasi wasijivune. (Selah)
משל בגבורתו עולם עיניו בגוים תצפינה הסוררים אל ירימו למו סלה׃
8 Mtukuzeni Mungu, enyi watu wa mataifa yote, sauti ya sifa zake isikike.
ברכו עמים אלהינו והשמיעו קול תהלתו׃
9 Yeye atuwekaye hai, naye hairuhusu miguu yetu iteleze.
השם נפשנו בחיים ולא נתן למוט רגלנו׃
10 Kwa maana wewe, Mungu, umetupima sisi, wewe umetupima kama inavyopimwa fedha.
כי בחנתנו אלהים צרפתנו כצרף כסף׃
11 Wewe ulituingiza sisi kwenye wavu; uliweka mzigo mzito viunoni mwetu.
הבאתנו במצודה שמת מועקה במתנינו׃
12 Wewe uliwafanya watu wasafiri juu ya vichwa vyetu; tulipita motoni na majini, lakini ukatuleta mahali pa wazi palipo salama.
הרכבת אנוש לראשנו באנו באש ובמים ותוציאנו לרויה׃
13 Nitaingia nyumbani mwako nikiwa na sadaka ya kuteketezwa; nitakulipa viapo vyangu
אבוא ביתך בעולות אשלם לך נדרי׃
14 ambavyo midomo yangu iliahidi na kinywa changu kiliongea nilipokuwa katika dhiki.
אשר פצו שפתי ודבר פי בצר לי׃
15 Nitakutolea sadaka ya kuteketezwa ya wanyama wanene pamoja na harufu nzuri ya kondoo waume; Nitatoa ng'ombe na mbuzi. (Selah)
עלות מחים אעלה לך עם קטרת אילים אעשה בקר עם עתודים סלה׃
16 Njoni, msikie, ninyi nyote mnao mwabudu Mungu, nami nitatangaza yale yeye aliyoitendea roho yangu.
לכו שמעו ואספרה כל יראי אלהים אשר עשה לנפשי׃
17 Nilimlilia kwa kinywa changu, naye alipendezwa na ulimi wangu.
אליו פי קראתי ורומם תחת לשוני׃
18 Kama ningelikuwa na dhambi ndani ya moyo wangu, Bwana asingenisikiliza.
און אם ראיתי בלבי לא ישמע אדני׃
19 Lakini Mungu hakika amesikia; amesikia sautiya kuomba kwangu.
אכן שמע אלהים הקשיב בקול תפלתי׃
20 Atukuzwe Mungu, ambaye hakuyakataa maombi yangu wala kuweka uaminifu wa agano lake mbali nami.
ברוך אלהים אשר לא הסיר תפלתי וחסדו מאתי׃

< Zaburi 66 >