< Zaburi 64 >
1 Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
to/for to conduct melody to/for David to hear: hear God voice my in/on/with complaint my from dread enemy to watch life my
2 Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
to hide me from counsel be evil from scheming to work evil: wickedness
3 Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
which to sharpen like/as sword tongue their to tread arrow their word bitter
4 ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
to/for to shoot in/on/with hiding complete suddenly to shoot him and not to fear
5 Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
to strengthen: hold to/for them word: deed bad: evil to recount to/for to hide snare to say who? to see: see to/for them
6 Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
to search injustice to finish plot to search and entrails: inner parts man and heart deep
7 Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
and to shoot them God arrow suddenly to be wound their
8 Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
and to stumble him upon them tongue their to wander all to see: see in/on/with them
9 Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
and to fear: revere all man and to tell work God and deed: work his be prudent
10 Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.
to rejoice righteous in/on/with LORD and to seek refuge in/on/with him and to boast: boast all upright heart