< Zaburi 64 >
1 Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
“For the leader of the music. A psalm of David.” Hear my voice, O God! when I pray! Preserve my life from the terrors of the enemy!
2 Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
Hide me from the assembly of the wicked, From the brawling crowd of evil-doers!
3 Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
For like a sword they sharpen their tongues, Like arrows they aim their poisoned words,
4 ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
To shoot in secret at the upright; Suddenly do they shoot at him without fear.
5 Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
They prepare themselves for an evil deed; They commune of laying secret snares: “Who,” say they, “will see them?”
6 Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
They meditate crimes: “We have finished,” say they, “our plans!” The heart and bosom of every one of them are deep.
7 Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
But God will shoot an arrow at them; Suddenly shall they be wounded.
8 Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
Thus their own tongues shall bring them down; All who see them will flee away.
9 Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
Then will all men stand in awe, And declare what God hath done, And attentively consider his work.
10 Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.
The righteous shall rejoice, and trust in the LORD; All the upright in heart shall glory.